Machapisho

WAZIRI MKUU: WATANZANIA TUNZENI AKIBA YA CHAKULA

Picha
  ..Ahimiza matumizi ya mbolea na mbegu za mazao ya muda mfupi. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka Watanzania watunze akiba ya chakula walichonacho na waepuke matumizi yasiyofaa kutokana na hali ya kuchelewa kwa msimu wa mvua. Waziri Mkuu ametoa wito huo leo jioni (Jumapili, Desemba 14, 2025) wakati akizungumza na baadhi ya Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, ofisini kwake Mlimwa, jijini Dodoma. Amewaeleza viongozi hao kutoka mikoa ya Dodoma na Singida kwamba Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ilitoa utabiri wa mwelekeo wa msimu wa mvua za vuli na mvua za msimu kwa kipindi cha Oktoba 2025 hadi Desemba 2025 na kipindi cha mwezi Novemba, 2025 hadi Aprili 2026 mtawalia.  “Kutokana na utabiri huo, baadhi ya mikoa nchini inatarajiwa kuwa na mvua za chini ya wastani hadi wastani na kutawaliwa na vipindi virefu vya ukavu na mtawanyiko wa mvua usioridhisha,” amesema.  Amesema tathmini hiyo ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inaonesha hali ya...

MHE. CHANDE AWAFUNDA WAHITIMU CHUO CHA USIMAMIZI WA WANYAMAPORI MWEKA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro. NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), amewataka wahitimu wa chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka, kuzingatia uadilifu, uzalendo na unyenyekevu wakati wa kuhudumia wananchi na kulinda rasilimali za wanyamapori ili kuongeza thamani katika maendeleo ya ukuaji wa sekta ya utalii kwa manufaa ya jamii na taifa kwa ujumla. Mhe. Chande ametoa wito huo mkoani Kilimanjaro wakati wa mahafali ya 61 ya chuo hicho kilichopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, ambapo amewasisitiza wahitimu hao kutumia vyema maarifa na taaluma ya elimu  waliyopata kufanya kazi kwa weledi na ufanisi mkubwa katika kuisaidia jamii kutatua changamoto zinazowakabili ikiwemo kusaidia kutatua migogoro baina ya binadamu na Wanyamapori wakali na waharibifu. “Vyeti tu havitoshi, bali utekelezaji wa yale mliyojifunza na kufunzwa chuoni, hivyo  nendeni kuyaonesha kwa vitendo huko mnapokwenda, kwa sababu cheti ni karatasi lakini maarifa mliyoyapata katika...

CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA LINDI MWAMBAO LTD CHAWEKA REKODI YA KUUZA TANI 41,000 ZA KOROSHO KATIKA MINADA MITANO

Picha
Na Lubango Mleka, Lindi. CHAMA Kikuu cha Ushirika cha Lindi Mwambao kimeendelea kufanya vizuri katika msimu wa mauzo ya korosho baada ya kupeleka sokoni jumla ya tani 41,000 katika minada mitano iliyofanyika tangu kuanza kwa msimu huu. Akizungumza mara baada ya kukamilika kwa mnada wa tano uliofanyika katika Halmashauri ya Mtama mkoani Lindi Mjumbe wa Bodi ya Lindi Mwambao Said Mwinyi amesema chama hicho kimeendelea kuhakikisha kuwa korosho za wanachama wake zinafika sokoni kwa wakati na kwa utaratibu unaotakiwa. Mwinyi amesema  katika minada yote mitano bei ya juu ya korosho imefikia shilingi 2,650 kwa kilo huku bei ya chini ikiwa shilingi 2,170 hatua ambayo amesema inaonesha utulivu wa soko na mwitikio mzuri kutoka kwa wanunuzi. “Hadi sasa tumeshapeleka sokoni zaidi ya tani 41,000 za korosho, jambo ambalo linaonesha uimara wa chama na maandalizi mazuri tuliyofanya. Wanachama wetu wanaendelea kunufaika na mchakato huu wa mauzo,” amesma Mwinyi.

ECOWAS YATARAJIA KUKUTANA HII LEO JIJINI ABUJA NIGERIA

Picha
JUMUIYA  ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi, ECOWAS inatarajiwa kukutana hii leo jijini Abuja nchini Nigeria, wakati huu ikitangaza hali ya hatari ya kikanda kufuatia kuongezeka kwa uongozi wa kijeshi na majaribio ya mapinduzi katika nchi za Mali, Burkina Faso, Niger, Guinea, na njama ya hivi punde zaidi nchini Benin ikitoa tahadhari mpya.

WAZIRI KIKWETE AAHIDI USHIRIKIANO KWA WATUMISHI WA WAKALA YA NDEGE ZA SERIKALI

Picha
  Na. Mwandishi Wetu-Dar es Salaam WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete ameipongeza Bodi, Menejimenti na Watumishi wa Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) kwa kuongoza na kusimamia Ndege za Serikali kwa weledi na  ufanisi mkubwa. Waziri Kikwete amesema hayo Desemba 12, 2025 jijini Dar es salaam wakati alipotembelea ofisi ya Wakala ya Ndege za Serikali (TGFA) kwa lengo la kujitambulisha. “Ninaipongeza Bodi kwa kuendelea kuwa washauri wazuri na kufanya uendelevu wa Wakala, binafsi ninaridhika na utendaji kazi wake. Pia Nitumie fursa hii kuwapongeza watumishi wote kwa ustadi wenu mkubwa wa kusimamia Ndege za Serikali, mimi na Naibu Waziri wa ofisi yangu Mhe. Regina Qwaray tunawahakikishia ushirikiano wa dhati wakati wote wa uongozi wetu” alisema Mhe. Kikwete. Aidha, Mhe. Kikwete amewapongeza kwa kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi ambao unaonekana kuridhisha viongozi wanawahudumia. Hivyo, ametoa rai pia kwa watu...

HALMASHAURI YA MONDULI YATUA HALMASHAURI YA JIJI LA DAR KUJIFUNZA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam. TIMU ya wataalamu kutoka Halmashauri ya wilaya ya Monduli mkoani Arusha ikiongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Happiness Laizer imefika katika Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kwa lengo kujifunza jinsi ya ukusanyaji wa mapato. Timu hiyo imepokelewa na mwenyeji wao Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji hilo ndugu Elihuruma Mabelya ambapo katika mazungumzo yake aliwaeleza wataalamu hao kuwa ufanisi wa ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam unachangiwa na ushirikiano wa watumishi katika kanda maalum za ukusanyaji mapato. Amesema uanzishwaji wa kanda hizo, umewezesha kuwasogezea wananchi huduma mbalimbali katika maeneo yao hali iliyochangia kuwapunguzia umbali wa kufuata huduma zikiwemo vibali mbalimbali, leseni n.k makao makuu ya Halmashauri.

SOMO LA LEO KUTOKA RSA TANZANIA

Picha
KWAmujibu wa kifungu cha 5(1)(e) cha Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) na Kanuni za LATRA za Usajili na Uthibitishaji Madereva na Wahudumu wa Mabasi (THE LAND TRANSPORT REGULATORY AUTHORITY (CERTIFICATION OF COMMERCIAL VEHICLE DRIVERS AND REGISTRATION OF CREW) REGULATIONS)) 2020, Dereva aliyesajiliwa na Kuthibitishwa na LATRA ana wajibu ufuatao kama sehemu ya masharti ya Kuthibitishwa kwake:  1. Kuzingatia mwendo kikomo (speed limits) uliowekwa barabarani kwa mujibu wa sheria; 2. Kutoendesha gari huku akiwa amelewa pombe au madawa ya kulevya; 3. Kuheshimu amri halali ya askari polisi au maafisa wa LATRA; 4. Kuendesha gari akiwa na leseni hai na cheti cha uthibitishwaji Kwa dereva anayeendesha gari la abiria, anatakiwa kuzingatia masharti yafuatayo ya ziada, kwa mujibu wa kanuni ya 10(2) ya kanuni tajwa hapo juu:  1. Kutopakia abiria Zaidi ya uwezo wa gari kama ulivyoandikwa kwenye cheti cha usajili wa/au leseni ya, gari; 2. Kuhakikisha milango imefungwa kab...

WAZIRI MKUU AKAGUA UKARABATI WA SOKO LA MAJENGO NA KUELEKEZA UKAMILIKE

Picha
Na Lubango Mleka, Dodoma WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ametembelea Soko la Majengo jijini Dodoma na kukagua maendeleo ya ukarabati wa soko hilo, ambapo amemuelekeza mkandarasi Kampuni ya Azhar Construction kukamilisha ukarabati huo ifikapo Mwezi Februari 2026 ili wafanyabiashara waanze kulitumia. Katika kuhakikisha maelekezo yake yanatekelezwa, Dkt. Mwigulu amemtaka Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko kufanya makubaliano ya kimaandishi na mkandarasi huyo kuwa, hakutakuwa na nyongeza ya muda wa ukarabati wa soko hilo ifikapo Mwezi Februari, 2026. “Serikali inataka ukarabati wa Soko ukamilike kwa wakati ili kukidhi mahitaji ya wakazi wa Jiji la Dodoma, ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira wezeshi ya kuendelea kukuza uchumi wa wafanyabiashara,” Dkt. Nchemba amesisitiza. Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe akimkaribisha Mhe. Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa ukarabati wa ...

GRUMETI FUND YAWEZESHA SAFARI KWA VIJANA WAWILI KUJIFUNZA NAMNA BORA YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA NCHINI TAIWAN

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Serengeti. SHIRIKA la Grumeti Fund kupitia Idara ya Maendeleo ya jamii, kituo cha Mazingira, limefadhili safari ya vijana wawili kutoka katika Shule za Sekondari Issenye na Natta za Wilayani Serengeti kwenda nchini Taiwan kwa ajili ya programu maalum ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu namna bora za utunzaji na uhifadhi wa mazingira.  Msimamizi wa Kituo cha Mazingira Bw. Laurian Kahatano amebainisha kuwa, Flora Nyaboko Gesimba, Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Natta na Mkazi wa Kijiji cha Maburi pamoja na Cosmas Godfrey Kitena, Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Issenye na Mkazi wa Kijiji cha Singisi wamepata ufadhili wa safari hiyo baada ya kuibuka washindi katika shindano la uandishi wa i insha (Essay) lililohusisha wanafunzi 32 kutoka katika shule 16 zilizopo kwenye program ya Elimu ya Mazingira inayoendeshwa kwenye kituo chetu cha Mazingira (EEC). "Hivi karibu tuliendesha mdahalo wa utunzi wa insha, katika shule zote 16 ambapo wanafunzi walipewa ...

WANAWAKE NKINGA HOSPITALI WAZINDUA KIKUNDI CHA KUSAIDIANA

Picha
Na Lubango Mleka, Nkinga - Igunga. WANAWAKE watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Nkinga jana Disemba 11, 2025 wamezindua rasmi kikundi chenye lengo la kusaidiana katika changamoto mbalimbali za kimaisha. Kikundi hicho kilichopewa jina la Nkinga Super Women Group kimezinduliwa katika Kikao cha kwanza cha Kufunga Mwaka, ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ndg.Victor Ntundwe alikuwa ndiye mgeni rasmi. "Ninawapongeza kwa kuunganisha nguvu ya pamoja katika kukabiliana na changamoto zenu, Siku zote Umoja ni nguvu, Uongozi wa hospitali unawathamini sana kwa jinsi mnavyoongoza wafanyakazi wengine kwa nidhamu, weledi na kuwa vinara wa huduma kwa mteja" amesema Mkurugenzi Ntundwe katika hotuba yake Bi.Epifania Nyaki ni mwenyekiti wa Umoja huo amesema, kuanzishwa kwa Umoja huo ni matokeo ya mawazo katika sherehe ya Siku ya Wanawake Duniani Machi, 2024 baada ya kushikwa mkono na Mkurugenzi wa Hospitali, na ndipo January 2025 kikundi hicho kikaanza rasmi. Ameongeza, kwasasa kikundi hich...

TANZIA

Picha
  SPIKA WA BUNGE LA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. MUSSA AZZAN ZUNGU (MB) ANASIKITIKA KUTANGAZA KIFO CHA MBUNGE WA PERAMIHO MHE. JENISTA JOAKIM MHAGAMA KILICHOTOKEA LEO 11,DESEMBA,2025 JIJINI DODOMA.

AMNESTY INTERNATIONAL YALISHUTUMU KUNDI LA HAMAS

Picha
SHIRIKA la Amnesty International limeishtumu Hamas na makundi mengine ya wapiganaji wa Kipalestina kwa mara ya kwanza kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu, ikiwemo mauwaji, wakati na baada ya shambulio la Oktoba 7, 2023 lililochochea vita vya Gaza. #HamasIsISIS ##palestine #AmnestyInternational

UJUMBE WA LEO KUTOKA RSA TANZANIA

Picha
   NDANI ya Jiji la Dar es Salaam au kwengineko ukiendesha kwa mwendo wa wastani wa kati ya 50-60Kph kwenye Zebra yoyote utaweza kusimama na kuwapisha wavukaji wavuke, ila spidi ikizidi hapo sio rahisi kusimama hasa mwenda kwa miguu anapotokea ghafla.  Hata hivyo, Jizoeshe Kusimama kwenye kila zebra kupisha watu wavuke, maana hata wewe ni mwenda kwa miguu ukitoka kwenye usukani.  Usiposimama kuwapisha, hawatakuwa na mahala pengine salama pa kuvuka zaidi ya kuhatarisha maisha yao.  Hivyo jambo la kwanza ondoa ile kasumba au mtazamo kuwa *Aagh wasumbufu hawa*, kwakuwa hata wao hao unaowaona kero wana haki ya kutumia barabara. Ni tofauti ya kipato tu au mazingira ya wakati huo ndio yamewafanya kwenda kwa miguu.  Na jinsi miji inavyozidi kukua ndivyo idadi ya watu inavyoongezeka huku kukiwa na miundo mbinu michache sana ya waenda kwa miguu, tegemea idadi kubwa ya waenda kwa miguu kila kwenye zebra. Hivyo kuwa mwenda kwa miguu sio dhambi.  Hii ndio sababu k...

AMUUA MWANAYE KWA KIPIGO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mbeya. MWANAMKE Mmoja  aitwaye ,Marry Timotheo mkazi wa kijiji cha Garijembe kata ya Tembela Wilaya ya Mbeya anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua kwa kumpiga na kitu kizito kichwani mtoto wake, Scola Mwaba(10)kwa madai ya kuzidi utukutu kisha mwili wake kutupa shamba lilo karibu na nyumbani anakoishi . Akizungumzia tukio hilo Desemba 10,2025 Kamanda wa Polisi Mkoani Mbeya, Benjamin Kuzaga amesema marehemu Scola alikuwa Mwanafunzi wa Darasa la Nne shule ya Msingi Ngonde wilaya ya Mbeya.  Kuzaga amesema kuwa tukio hilo limetokea Desemba 9,2025 ,majira ya saa 6.30 mchana katika Kijiji cha Garijembe ,Kata na Tarafa ya Tembela  Wilaya ya Mbeya. "Mama wa marehemu alimshambulia kwa kitu kizito kichwani  mtoto wake kwa madai ya kuzidi utukutu kisha mwili wake kutupa jirani na shamba la nyumba anakoishi "amesema Kamanda Kuzaga.  Aidha Kuzaga ameeleza kuwa pia licha ya  kumshikilia mama wa marehemu ,pia  jirani yake ,Sharifa Nz...