Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba 12, 2025

HALMASHAURI YA MONDULI YATUA HALMASHAURI YA JIJI LA DAR KUJIFUNZA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam. TIMU ya wataalamu kutoka Halmashauri ya wilaya ya Monduli mkoani Arusha ikiongozwa na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi. Happiness Laizer imefika katika Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam kwa lengo kujifunza jinsi ya ukusanyaji wa mapato. Timu hiyo imepokelewa na mwenyeji wao Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji hilo ndugu Elihuruma Mabelya ambapo katika mazungumzo yake aliwaeleza wataalamu hao kuwa ufanisi wa ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam unachangiwa na ushirikiano wa watumishi katika kanda maalum za ukusanyaji mapato. Amesema uanzishwaji wa kanda hizo, umewezesha kuwasogezea wananchi huduma mbalimbali katika maeneo yao hali iliyochangia kuwapunguzia umbali wa kufuata huduma zikiwemo vibali mbalimbali, leseni n.k makao makuu ya Halmashauri.

SOMO LA LEO KUTOKA RSA TANZANIA

Picha
KWAmujibu wa kifungu cha 5(1)(e) cha Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) na Kanuni za LATRA za Usajili na Uthibitishaji Madereva na Wahudumu wa Mabasi (THE LAND TRANSPORT REGULATORY AUTHORITY (CERTIFICATION OF COMMERCIAL VEHICLE DRIVERS AND REGISTRATION OF CREW) REGULATIONS)) 2020, Dereva aliyesajiliwa na Kuthibitishwa na LATRA ana wajibu ufuatao kama sehemu ya masharti ya Kuthibitishwa kwake:  1. Kuzingatia mwendo kikomo (speed limits) uliowekwa barabarani kwa mujibu wa sheria; 2. Kutoendesha gari huku akiwa amelewa pombe au madawa ya kulevya; 3. Kuheshimu amri halali ya askari polisi au maafisa wa LATRA; 4. Kuendesha gari akiwa na leseni hai na cheti cha uthibitishwaji Kwa dereva anayeendesha gari la abiria, anatakiwa kuzingatia masharti yafuatayo ya ziada, kwa mujibu wa kanuni ya 10(2) ya kanuni tajwa hapo juu:  1. Kutopakia abiria Zaidi ya uwezo wa gari kama ulivyoandikwa kwenye cheti cha usajili wa/au leseni ya, gari; 2. Kuhakikisha milango imefungwa kab...

WAZIRI MKUU AKAGUA UKARABATI WA SOKO LA MAJENGO NA KUELEKEZA UKAMILIKE

Picha
Na Lubango Mleka, Dodoma WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ametembelea Soko la Majengo jijini Dodoma na kukagua maendeleo ya ukarabati wa soko hilo, ambapo amemuelekeza mkandarasi Kampuni ya Azhar Construction kukamilisha ukarabati huo ifikapo Mwezi Februari 2026 ili wafanyabiashara waanze kulitumia. Katika kuhakikisha maelekezo yake yanatekelezwa, Dkt. Mwigulu amemtaka Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Dkt. Frederick Sagamiko kufanya makubaliano ya kimaandishi na mkandarasi huyo kuwa, hakutakuwa na nyongeza ya muda wa ukarabati wa soko hilo ifikapo Mwezi Februari, 2026. “Serikali inataka ukarabati wa Soko ukamilike kwa wakati ili kukidhi mahitaji ya wakazi wa Jiji la Dodoma, ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira wezeshi ya kuendelea kukuza uchumi wa wafanyabiashara,” Dkt. Nchemba amesisitiza. Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe akimkaribisha Mhe. Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema kuwa ukarabati wa ...

GRUMETI FUND YAWEZESHA SAFARI KWA VIJANA WAWILI KUJIFUNZA NAMNA BORA YA UTUNZAJI WA MAZINGIRA NCHINI TAIWAN

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Serengeti. SHIRIKA la Grumeti Fund kupitia Idara ya Maendeleo ya jamii, kituo cha Mazingira, limefadhili safari ya vijana wawili kutoka katika Shule za Sekondari Issenye na Natta za Wilayani Serengeti kwenda nchini Taiwan kwa ajili ya programu maalum ya kujifunza na kubadilishana uzoefu kuhusu namna bora za utunzaji na uhifadhi wa mazingira.  Msimamizi wa Kituo cha Mazingira Bw. Laurian Kahatano amebainisha kuwa, Flora Nyaboko Gesimba, Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Natta na Mkazi wa Kijiji cha Maburi pamoja na Cosmas Godfrey Kitena, Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Issenye na Mkazi wa Kijiji cha Singisi wamepata ufadhili wa safari hiyo baada ya kuibuka washindi katika shindano la uandishi wa i insha (Essay) lililohusisha wanafunzi 32 kutoka katika shule 16 zilizopo kwenye program ya Elimu ya Mazingira inayoendeshwa kwenye kituo chetu cha Mazingira (EEC). "Hivi karibu tuliendesha mdahalo wa utunzi wa insha, katika shule zote 16 ambapo wanafunzi walipewa ...

WANAWAKE NKINGA HOSPITALI WAZINDUA KIKUNDI CHA KUSAIDIANA

Picha
Na Lubango Mleka, Nkinga - Igunga. WANAWAKE watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Nkinga jana Disemba 11, 2025 wamezindua rasmi kikundi chenye lengo la kusaidiana katika changamoto mbalimbali za kimaisha. Kikundi hicho kilichopewa jina la Nkinga Super Women Group kimezinduliwa katika Kikao cha kwanza cha Kufunga Mwaka, ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ndg.Victor Ntundwe alikuwa ndiye mgeni rasmi. "Ninawapongeza kwa kuunganisha nguvu ya pamoja katika kukabiliana na changamoto zenu, Siku zote Umoja ni nguvu, Uongozi wa hospitali unawathamini sana kwa jinsi mnavyoongoza wafanyakazi wengine kwa nidhamu, weledi na kuwa vinara wa huduma kwa mteja" amesema Mkurugenzi Ntundwe katika hotuba yake Bi.Epifania Nyaki ni mwenyekiti wa Umoja huo amesema, kuanzishwa kwa Umoja huo ni matokeo ya mawazo katika sherehe ya Siku ya Wanawake Duniani Machi, 2024 baada ya kushikwa mkono na Mkurugenzi wa Hospitali, na ndipo January 2025 kikundi hicho kikaanza rasmi. Ameongeza, kwasasa kikundi hich...