Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 22, 2026

NYANSAHO FOUNDATION YAZIDI KUHAMASISHA MAENDELEO BILLION 1.4 ZAKUSANYWA KWENYE HARAMBEE KIJIJI CHA MUSATI WILAYANI SERENGETI.

Picha
Na Jovina Massano, Serengeti.  KATIKA kuhakikisha jamii inapata huduma muhimu karibu na maeneo yao Nyansaho Foundation na wadau mbalimbali  wachangia Shillingi Billioni 1.4 zitakazowezesha upatikanaji wa huduma za afya na elimu Kijiji cha Musati. Harambee hiyo imefanyika hivi karibuni katika Kijiji cha Musati wilayani Serengeti mkoani Mara ambapo ilitanguliwa na uzinduzi wa kanisa la Waadventista wa Sabato- Musati Central na nyumba ya mchungaji ambavyo vyote kwa pamoja vimejengwa kwa ufadhili wa taasisi ya Nyansaho  kwa kiasi cha millioni 500. Akiongoza harambee hiyo Waziri wa Ujenzi ,Mh.Abdalah Ulega(MB) ameweza kukusanya jumla ya Shillingi Billioni 1.4 zitakazowezesha kujenga Shule pamoja na Zahanati katika Kijiji hicho. Katika harambee hiyo Waziri Ulega na rafiki zake wamechangia shillingi millioni 100 na kuongoza uchangiaji kutoka kwa wadau mbalimbali wa Maendeleo (wafanyabiashara) zikiwemo taasisi za fedha, wageni waalikwa na wananchi na kuweza kufikisha kiasi hicho ...

TABASAMU LA MATUMAINI: WANAFUNZI 16 KIFUBATA WAPATA NGUVU MPYA YA KUSOMA.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Igunga.  KUNA nyakati ambapo msaada mdogo hugeuka kuwa mwanga mkubwa wa matumaini. Hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa wanafunzi 16 wanaoishi katika mazingira magumu wa Shule ya Sekondari Kifubata, Kata ya Nkinga, Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, baada ya kupokea msaada wa vifaa vya shule uliolenga kubadili simulizi ya changamoto zao za kila siku. Msaada huo umejumuisha mahitaji muhimu kama madaftari, kalamu, mabegi ya shule, masweta na sare, vitu ambavyo kwa wengi vinaweza kuonekana vya kawaida, lakini kwa wanafunzi hawa ni daraja muhimu kuelekea ndoto zao za kielimu. Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa taasisi ya Nkinga and Save Care Organisation, Edina Kalibate, alisisitiza umuhimu wa mshikamano wa jamii katika kusaidia makundi yenye uhitaji. "Mbunge wetu amekuwa akishirikiana kwa karibu na taasisi yetu kuwafikia watoto wenye mahitaji maalum pamoja na jamii inayowazunguka. Ushirikiano wa kila mmoja ni muhimu ili kuleta mabadiliko ya kweli,...