Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 31, 2026

BONANZA LA MICHEZO TASAC LAFANA

Picha
  Na Lubango Mleka, Dar Es Salaam. SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) leo, tarehe 31 Januari 2026, limefanya Bonanza la Michezo  katika viwanja vya APC Bunju, kwa lengo la kuimarisha afya, mshikamano, na mahusiano mema kazini. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Bonanza hilo, Mkurugenzi Mkuu wa TASAC, Bw. Mohamed Salum, aliwataka watumishi wote waliohudhuria kuendeleza tabia ya kufanya mazoezi kama njia ya kujenga na kuimarisha afya. "Nipende kuchukua nafasi hii kuwakaribisha watumishi wote mliojitokeza katika Bonanza hili la Michezo. Ushiriki wenu unaonesha mshikamano na umoja tulionao kama familia moja ya Shirika. Bonanza hili liwe chachu ya kuendeleza utamaduni wa michezo ndani ya Shirika letu.” Alisema Bw. Salum. Bw. Salum ametoa rai kwa watumishi hao kujibidiisha kwa kushiriki mic zo na mazoezi ya viungo mara kwa mara, kwani michezo ni nguzo muhimu katika kujenga na kuimarisha afya, kuongeza ufanisi kazini na kuimarisha mahusiano mema miongoni mwa wafanyakazi wa TA...

MICHEZO NI SILAHA YA UMOJA, AFYA NA TIJA KAZINI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mwigulu Nchemba, amesema michezo ni nyenzo muhimu katika kuondoa mipasuko ya kijamii, kuimarisha mahusiano ya kikazi na kuongeza tija katika taasisi za umma na binafsi, akisisitiza kuwa mchango wake unaenda mbali zaidi ya burudani au mazoezi ya mwili. Akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri Mkuu katika Bonanza la Bunge lililofanyika jijini Dodoma kwa ufadhili wa Benki ya Azania, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukivi, amesema michezo imeendelea kuthibitisha nafasi yake kama nguzo ya mshikamano, umoja na maendeleo ya Taifa. Ameeleza kuwa pamoja na kujenga afya ya mwili, michezo ni njia madhubuti ya kupunguza msongo wa mawazo, kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari na shinikizo la damu, pamoja na kuimarisha afya ya akili kwa watumishi na jamii kwa ujumla. “Msingi wa Bonanza la Bunge ni kuhimiza mshikamano na ushiriki wa jamii. Ushirikishwaji wa wabunge, watumishi wa Bunge, taasisi za S...

SERIKALI YATOA VIFAA VYA KIDIJITI BILIONI 5.4 KUWAWEZESHA WALIMU WENYE ULEMAVU

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imenunua na kusambaza vifaa vya kidijiti na saidizi vyenye thamani ya shilingi bilioni 5.4 kwa walimu wa shule za msingi na sekondari, wakufunzi pamoja na walimu tarajali wenye ulemavu katika vyuo vya ualimu nchini, kwa lengo la kurahisisha ujifunzaji na ufundishaji jumuishi. Akizungumza na waandishi wa habari Januari 31, 2026 jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi za Rais Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100, akisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imejizatiti kuhakikisha wanafunzi na walimu wenye mahitaji maalum hawatengeki katika mfumo wa elimu. Prof. Mkenda amesema jumla ya wanufaika 1,055 kutoka Halmashauri 104 nchini wamenufaika na mpango huo, ambapo vifaa vilivyosambazwa ni pamoja na kompyuta mpakato 680, vifaa tisa vya Brain Note Touch Pass, vinasa sauti (voice recorders) 377, tablet 196 kwa wana...