WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) YASHIRIKI TAMASHA LA KILIMO JIJINI MBEYA.
Wahamasisha Nishati Safi ya Kupikia. Na Mwandishi Wetu, Iwambi- Mbeya. WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) unashiriki katika tamasha la kilimo linalofanyika katika viwanja vya Iwambi jijini Mbeya kuanzia tarehe 25 mpaka 29 Aprili 2026, ambapo zaidi ya watu 100,000 wakiwemo vijana kutoka mikoa mbalimbali ya kanda ya nyanda za juu kusini wanatarajiwa kushiriki. Wakala unatumia jukwaa hilo kuelimisha na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi pamoja na kueleza hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme katika maeneo ya vijijini. Kupitia banda lake, REA imeonesha bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia, ambapo bidhaa kuu zinazohamasishwa ni pamoja na matumizi ya majiko ya umeme, majiko ya gesi pamoja na majiko banifu. Teknolojia hizo zimebainishwa kuwa suluhisho muhimu katika kupunguza matumizi ya nishati chafu kama kuni na mkaa, kulinda mazingira na kuboresha afya za watumiaji. Akifungua rasmi maonesho hayo, Kaimu mkuu wa wilaya ya Mbeya ambae pia ni Mk...