Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba 5, 2025

KALEYA MOLLEL ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA SIMANJIRO

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro DIWANI wa Kata ya Msitu wa Tembo, Kaleya Melita Mollel amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, kwa kura zote 24 za Madiwani waliohudhuria kikao. Mwakilishi wa Katibu Tawala wa wilaya ya Simanjiro, Edosi Evaristi Ndikwiki amesema Mollel ambaye ni Diwani wa Kata ya Msitu wa Tembo, amepata kura zote 24 zilizopigwa  Ndikwiki pia amesema, madiwani hao wamemchagua Diwani viti maalum wa Tarafa ya Terrat, Mwanjaa Jacob kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa kura zote 24 za ndiyo. Amesema katika uchaguzi huo uliofanyika  mji mdogo wa Orkesumet ulihusisha madiwani wote wanaotokana na CCM wa kata zote 18 na viti maalumu sita. Ndikwiki amewaasa madiwani hao kutoa ushirikiano kwa wataalam wa halmashauri hiyo kwani wameshaapa kutumikia nafasi zao. "Tuzingatie mahusiano mazuri na watumishi, tuwape ushirikiano na tuwe watatuzi wa migogoro tusiibue migogoro ambayo itaturudisha nyu...

WANANCHI BABATI WAIPA KONGOLE REA

Picha
Mitungi ya gesi 3,255 kusambazwa  na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Mitungi mmoja kuuzwa kwa bei ya ruzuku TZS 17,500. Na Mwandishi Wetu, Babati. Kongole hizo zimetolewa leo, tarehe 04 Disemba, 2025 na wananchi wa kata ya Ayalagaya Wilaya ya Babati mkoani manyara wakati wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku katani hapo. Uuzaji wa majiko hayo umeongozwa na  diwani wa kata ya Ayalagaya Mheshimiwa Sabil John , mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Babati, mtendaji kata ya Ayalagaya , Afisa kutoka REA na mwakilishi wa kampuni Manjis Logistics Limited.  "Kinachofanyika leo ni kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia  katika kutunza mazingira na afya za wananchi" amesema Mhe. Sabil. Mhe. Sabil amesema, Lengo la mradi huu unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni kuendeleza juhudi za utunzaji wa mazingira na Afya za wananchi kwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu  na hamasa ya ...