Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi 26, 2026

MMOJA AFARIKI, WAWILI WAJERUHIWA WAKIBISHANIA SIMBA NA YANGA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mwanza.  MTU mmoja amefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa baada ya kutokea ugomvi uliozuka kutokana na ushabiki wa mpira kati ya mashabiki wa timu za Simba na Yanga Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza. Kwa mujibu taarifa iliyotolewa leo na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, DCP Wilbrod Mutafungwa amesema tayari wameanzisha msako wa kumtafuta kijana mmoja (jina limehifadhiwa) kwa tuhuma za kumuua Abel Mganga Mazuri (25) mkazi wa Nyamahengo, na kuwajeruhi watu wawili kufuatia ugomvi uliotokana na ushabiki wa mpira. Taarifa hiyo imesema tukio hilo limetokea Machi 24, 2026 majira ya saa 5:30 usiku katika kitongoji cha Nyamahengo, kijiji na kata ya Sumve, wilayani Kwimba, mkoani Mwanza. "Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limeanza msako wa kumtafuta kijana mmoja (jina limehifadhiwa kwa sasa) kwa tuhuma za mauaji ya Abel Mganga Mazuri, miaka25, mkazi wa Nyamahengo aliyeuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali kifuani kisha kuwajeruhi watu wawili kwa kutumia kitu c...

FDC URAMBO WAJIVUNIA MAFANIKIO MAKUBWA

Picha
  Na Allan Kitwe, Urambo.  CHUO Cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Urambo kimeishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha miundombinu na kukipatia vifaa vya mafunzo ambavyo vimekiongezea mapato. Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa Chuo hicho Elias Niima alipokuwa akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake ambapo alieleza kufurahishwa na uamuzi wa serikali ya Awamu ya Sita kukifanyia maboresho makubwa chuo hicho.   Amesema kuwa kipindi cha miaka 4 ya Uongozi wa Rais Samia na siku 100 za awamu yake ya pili tangu aingie madarakani, chuo kimepata mafanikio makubwa ikiwemo kuzalisha samani za taasisi mbalimbali na kuingiza mapato. Ametaja baadhi ya samani zilizotengenezwa kuwa ni madawati, viti na meza zaidi ya 7,000 kwa shule za msingi na sekondari za halmashauri za Wilaya ya Urambo na 2,500 za halmashauri ya Wilaya ya Kaliua. ‘Miradi hii imetekelezwa na Chuo kwa kutumia nguvu kazi ya wanafunzi na walimu wao, ikiwa ni sehe...