Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 10, 2026

SALALI: AIPONGEZA SERIKALI KUANDA SERA INAYOZINGATIA MAKUNDI MAALUM

Picha
  Na Carlos Claudio, Dodoma. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Foundation Disability Hope (FDH), Maiko Salali, ameipongeza serikali kwa kuandaa sera jumuishi inayozingatia makundi maalum, ikiwemo watu wenye ulemavu, hatua aliyoieleza kuwa ni muhimu katika kukuza usawa wa kijamii na kiuchumi nchini. Akizungumza leo Jumatano, 2026, katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Mnyororo wa Ugavi ya Mwaka 2025, Salali alisema sera hiyo imezingatia kwa kiasi kikubwa dhana ya ujumuishwaji. Alieleza kuwa utekelezaji wa sheria ya ununuzi wa umma inayotenga asilimia 30 kwa makundi maalum umeendelea kufungua milango ya fursa kwa watu wenye ulemavu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi. “Tumeridhishwa na namna sera hii ilivyozingatia ujumuishwaji. Hata watu wenye ulemavu wa kuona wamewezeshwa kuipata sera hii kupitia maandishi ya nukta nundu,” alisema Salali. Aidha, alibainisha kuwa uongozi wa Rais S...

WADAU WA KILIMO WAOMBA SERIKALI KUONDOA KODI YA ONGEZEKO (VAT)

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WADAU wa Kilimo wameiomba serikali kuondoka kodi ya ongezeko la thamani (VAT) ya asilimia 18 kwenye mifuko ya tabaka ya kuhifadhia mazao ya nafaka na mbegu ili kuwesha wakulima kuongeza kipato na usalama wa chakula. Hayo yalielezwa Jijini Dodoma  na Afisa Mradi Jukwaa la Wadau wa Kilimo wasiokuwa wa Kiserikali (ANSAF)  Werner Hillary wakati akifungua warsha ya kujadili maboresho ya kisera ili kudhibiti changamoto za upotevu kwa wakulima wadogo kwa kushirikiana na Shirika la Helvetas. " Warsha hii ilitohusisha wadau mbalimbali wa Kilimo ikiwemo Serikali, wazalishaji wadogo na Asasi za Kiraia ni sehemu ya mradi unaotekelezwa kwa ushirikiani wa Helvetas Tanzania, SAT, Chuo cha Kilimo SUA na Chuo Kikuu cha Zurich. Afisa huyo amesema lengo la wadau kuiomba Serikali kuondoa kodi ya VAT ni kuwezesha wakulima wadogo kuwa na uwezo wa kununua na kutumia mifuko hiyo inayozuia wadudu waharibifu na upotevu wa nafaka. "Matumizi ya mifuko ya tabaka hus...