Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti 4, 2025

MHE. DOTTO BITEKO ASHINDA KWA ASILIMIA 99.8

Picha
IDADI YA WAPIGA KURA JIMBO LA BUKOMBE - GEITA NI 7,845.  = Wajumbe waliohudhuria 7456.  = Wajumbe wasiohudhuria 389.  Idadi ya kura zilizopigwa 7456.  = Idadi ya kura zilizoharibika 15.  = Idadi ya kura halali 7441.  ✅ KURA ZA NDIO 7441.  = KURA ZA HAPANA 00.  *WASTANI WA WAPIGA KURA WALIOJITOKEZA NI ASILIMIA 95.04.  *WASTANI WA USHINDI NI ASILIMIA 99.8. @BUKOMBE @BITEKO @CCMTAIFA

WASIMAMIZI WASAIDIZI NGAZI YA KATA JIMBO LA MANONGA NA IGUNGA WATAKIWA KUENDELEZA UTENDAJI WAO KIUADILIFU. MSIMAMIZI wa

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga.  MSIMAMIZI wa Uchaguzi Jimbo la Igunga na Manonga wilayani Igunga mkoani Tabora, Hamisi Hamisi amewaasa Wasimamizi Wasaidizi ngazi ya kata kuendeleza utendaji wao wa kiuadilifu, uaminifu, uzalendo, uchapakazi na uaminifu. Hamisi ametoa rai hiyo wakati wa mafunzo kwa Wasimamizi hao yaliyofanyika katika ukumbi wa Maxweli mjini Igunga. “Nyinyi mliopo hapa mmeteuliwa kwa mujibu wa sheria, hivyo mnaowajibu wa kikatiba na sheria kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani katika maeneo yenu’’ amesisitiza. Aidha, amewakumbusha wamebeba dhamana kubwa, nyeti na muhimu kwa mustakabali wa Tanzania Bara, hivyo wanategemewa kuzingatia utendaji wao na kuwajibika ipasavyo kipindi chote cha utumishi wao katika Tume Huru ya Uchaguzi.

MATUKIO KATIKA PICHA.

Picha
 Wajumbe wa CCM Kata ya Igunga wakiwa katika zoezi la upigaji kura ya maoni kwa nafasi ya Ubunge na Udiwani linalo endelea  katika ukumbi wa Sakao Igunga mjini .

MATUKIO KATIKA PICHA.

Picha
 Katibu wa Jumuia ya Wazazi CCM Wilaya ya Igunga Bi. Aziza Kiyabo ambaye ni Msimamizi wa Uchaguzi Kura za Maoni Kata ya Igunga akitoa maelekezo kwa Wajumbe kabla ya ziezi la upigaji kura za maoni kuanza.

HABARI PICHA KUTOKA UKUMBI WA SAKAO IGUNGA

Picha
  WAJUMBE KUTOKA MATAWI 9 YA KATA YA IGUNGA WAKIWA TAYARI KUPIGA KURA YA MAONI KUPATA MBUNGE NA MADIWANI KWA TIKETI YA CCM JIMBO LA IGUNGA.