*Majiko banifu 4,836 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku mkoa wa Njombe. Jiko moja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya TZS 8,850 tu. 📌 *Kila walaya kupata majiko 1,209* Na Mwandishi Wetu, Njombe. KATIBU Tawala wa Mkoa wa Njombe Bi. Judica Omari amekutana na Timu ya Wataalam kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) leo Septemba 1, 2025 na kupata taarifa ya mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku ambao unatarajia kuanzia mapema mwezi wa 9, 2025. Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Mhandisi wa miradi Kutoka wakala wa Nishati Vijijini, Raya Majallah, amesema, Wakati Taifa likiwa kwenye mkakati wa kuhakikisha Watanzania wanatumia nishati safi na salama ya kupikia, Wakala wa Nishati Vijijini umekuja na mpango wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu 200,000 kwa bei ya ruzuku yanayotumia kuni na mkaa mchache sana na yenye ufanisi mkubwa katika matumizi yake. Mradi huu umekuja kwa lengo la kuimarisha na kubor...