Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 21, 2026

SERIKALI, WADAU WAWEKA MIKAKATI KUKABILI VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI

Picha
  Na WAF, Dodoma. Serikali kupitia Wizara ya Afya, Idara ya Afya ya Uzazi wa Mama na Mtoto, kwa kushirikiana na Shirika la Thamini Uhai wamekutana pamoja na kuweka mikakati utekelezaji wa Mradi wa Ushirikiano wa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.  Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto, Dkt. Ahmad Makuwani wakati wa kikao hicho kilichofanyika leo Januari 21, 2026 katika Ofisi za Wizara ya Afya Mtumba jijini Dodoma. "Serikali imeweka nia ya dhati ya kuhakikisha inaendelea kuweka mikakati madhubuti ya kupunguza idadi ya vifo vitokanavyo na uzazi kwa kushirikisha wadau mbalimbali ili kufanikisha utekelezaji wa mradi huo," amesema Dkt. Makuwani. Ameongeza kuwa ni muhimu kwa Wizara ya Afya kupitia Idara ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto ikuweka mikakati bora ya namna ya kutekeleza mradi huo ikiwa ni pamoja na kuangalia maeneo yanayopaswa kupewa kipaumbele katika mradi huo ikiwemo ujenzi wa majengo ya uangalizi maalum wa mtoto wenye changamoto mba...

POLISI WAKANUSHA TAARIFA YA CHADEMA "HATUJAKAMATA MTU YEYOTE NKASI"

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Rukwa. JESHI la Polisi Mkoa wa Rukwa leo Jumatano Januari 21, 2026 limekanusha taarifa zisizo sahihi zilizosambazwa mitandaoni zikidai kuwa Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA wamevamiwa, kukamatwa na kutawanywa kwa nguvu na Jeshi la Polisi wakati wakipanda Miti Wilayani Nkasi, Mkoani Rukwa. Kupitia taarifa yake kwa Vyombo vya habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa amesema taarifa hizo za CHADEMA hazina ukweli wowote na zina lengo la kupotosha na kuzua taharuki zisizo na msingi kwani katika Wilaya ya Nkasi na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla hakuna tukio la matumizi ya mabavu ama la wafuasi wa Chama hicho kukamatwa na Jeshi la Polisi. "Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa linaendelea kuimarisha usalama wa raia na mali zao na tunaendelea kusisitiza wananchi kupuuza taarifa zinazoandaliwa na kusambazwa kwa lengo la kupotosha, kuchonganisha, kujenga chuki baina ya wananchi na Taasisi mbalimbali." Imesema taarifa hiyo ya Polisi. Jana kupitia Mitandao...

SERIKALI KUPANUA UTAFITI WA MADINI YA KINYWE KWA USHIRIKIANO NA MAREKANI

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. SERIKALI imetangaza mpango wa kupanua utafiti wa kina wa Madini ya Kinywe kwa kushirikiana na Serikali ya Marekani, hatua inayolenga kuongeza maarifa ya kitaalamu na kubaini fursa mpya za maendeleo katika sekta ya madini. Akizungumza jijini Dodoma, Waziri wa Madini Anthony Mavunde amesema ushirikiano huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuhakikisha rasilimali za madini zinatambulika kikamilifu na kutumika kwa manufaa ya Taifa na wananchi. Mavunde amesema maeneo ya awali yaliyofanyiwa utafiti yanaonesha uwepo wa Madini ya Kinywe katika mikoa ya Lindi na Mtwara, na kwamba Serikali itaendelea kupanua wigo wa utafiti ili kupata takwimu kamili za kijiolojia. Ameeleza kuwa Watanzania wanaomiliki leseni za uchimbaji wa madini watapewa kipaumbele katika mpango huo, ambapo Serikali itashirikiana na wataalamu wa Marekani kufanya uchambuzi wa kina wa rasilimali hizo. Kwa mujibu wa Waziri huyo, jitihada hizo zinatarajiwa kuongeza uzalishaji wa madini hayo kwa s...

WAWILI WAFUNGWA MIAKA 30 KWA UBAKAJI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro. WAKAZI wawili wa mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 jela kwa kumbaka kwa zamu msichana mwenye umri wa miaka 24. Pamoja na kumbaka na kumwingilia kinyume cha maumbile msichana huyo pia walimpora simu aina ya Samsung na kumwibia fedha zake Sh70,000. Hata hivyo, katika hukumu ya kesi hiyo namba 10374/2025 iliyotolewa mji mdogo wa Orkesumet na hakimu wa mahakama ya wilaya hiyo Nicodemo washtakiwa watatu kati ya watano hawakuwepo mahakama hapo.  Hakimu Nicodemo amewataja washtakiwa Meshack Paulo (23) na Ibrahim Ibu (24) ambao ni wachimbaji wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani walimbaka, kumlawiti  Amesema washtakiwa hao na wenzao watatu Februari 4, 2025 kwa pamoja walimbaka msichana huyo ambaye ni muhudumu wa bar ya Feri mwenye umri wa miaka 24. Ameeleza kwamba wakati msichana huyo usiku huo wa saa 8 akitoka kazini akitembea kwenda nyumbani alimuona mshtakiwa wa kwanza Meshack akiwa...

TARURA YATENGA BIL 7 KUTENGENEZA KM 114 ZA BARABARA TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. WAKALA wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoani Tabora wanatarajia kutengeneza barabara zenye urefu wa km 114.05 kwa gharama ya sh bilioni 7.4 katika Wilaya ya Tabora Mjini kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Hayo yamebainishwa jana na Meneja wa Wakala huo Wilaya ya Tabora, Mhandisi Subira Manyama alipokuwa akiwasilishwa rasimu ya mapendekezo ya bajeti ya TARURA kwa mwaka wa fedha 2026/2027. Ametaja vipaumbele vya rasimu hiyo kuwa ni kukarabati barabara zote ambazo zimekuwa hazipitiki kwa kipindi kirefu ili ziweze kupitika wakati wote, kuzifanyia matengenezo barabara zote za mjini na vijijini ili ziwe imara zaidi. Ameongeza kuwa watafanya matengenezo ya kawaida kwa sehemu korofi zote na ya muda maalumu kwa baadhi ya barabara ili kuwezesha wananchi kusafiri na kusafirisha mazao yao kutoka vijijini kwenda kwenye masoko kwa mwaka mzima. Mhandisi Manyama amefafanua kuwa kwa mwaka wa fedha 2026/2027 wanatarajia kutumia kiasi cha sh bil 7.4 kwa ajili ya maten...

SERIKALI YATAKA CBE KUZALISHA WATAALAMU BUNIFU KUSAIDIA SEKTA YA UTALII

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro. SERIKALI imekitaka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kuelekeza nguvu katika kuzalisha wataalamu wabunifu na wenye ujuzi wa hali ya juu watakaoweza kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya utalii, ikiwa ni sehemu ya mkakati mpana wa kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. Kauli hiyo imetolewa  na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe Dennis Londo (Mb.) akiwa ameambatana na Viongozi mbalimbali wakati wa ziara yake ya kukagua eneo linalotarajiwa kujengwa Kampasi ya CBE Kilimanjaro lililopo wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro. Amesema kampasi hiyo inatarajiwa kuwa sehemu ya majibu ya changamoto za kimuundo na kitaalamu zinazokabili sekta ya utalii, kwa kuandaa wataalamu watakaobobea katika biashara ya utalii na shughuli zote zinazohusiana, ikiwemo ukarimu, ujasiriamali, masoko ya utalii na usimamizi wa biashara za utalii. “Tunatambua umuhimu mkubwa wa sekta ya utalii katika mapato ya Taifa na ajira, ndio maana tunataka CBE izalishe wataalamu watak...

KAPINGA ACHANGIA VIFAA VYA UJENZI SHULE ZA MSINGI UGANO NA KIBANDAI A – MBINGA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mbinga. MBUNGE wa Jimbo la Mbinga Vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga amechangia vifaa vya ujenzi kwa Shule ya Msingi Ugano iliyopo Kata ya Kambarage na Shule ya Msingi Kibandai A iliyopo Kata ya Maguu, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, mkoani Ruvuma, kwa lengo la kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia. Mchango huo umehusisha bati 100 za geji 28 zenye thamani ya shilingi milioni 3.5 kwa ajili ya kuezeka vyumba viwili vya madarasa, mbao za kenchi zenye thamani ya shilingi milioni 1, pamoja na mifuko ya saruji na nondo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyumba katika Shule ya Msingi Ugano. Akiwa katika Kijiji cha Kibandai A, Kata ya Maguu, Mhe. Kapinga amesema anatambua changamoto za uchakavu wa miundombinu ya shule ikiwemo madarasa, nyumba za walimu, nyumba ya mganga pamoja na ofisi za shule, na ameahidi kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga kuzitatua changamoto hizo, Katika hatua hiyo, Mhe. Kapinga amechangia mifuko...

NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAPIGA HODI SIMANJIRO.

Picha
  Mitungi ya gesi 3,255 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku, Mtungi mmoja kuuzwa kwa bei ya ruzuku ya shilingi 17,500. Na Mwandishi Wetu, Simanjiro. WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) leo jumatano ya tarehe 21 Januari , 2026 umeendelea na usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara Uuzaji na usambazaji umefanyika katika kata ya Mirerani maeneo ya ofisi ya mamlaka ndogo ya mji wa Mirerani. Akizungumza wakati wa uuzaji wa mitungi hiyo msimamizi wa mradi kutoka REA, ndugu Abdulrazack Mkomi Amesema, Usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia uliozinduliwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mwezi Mei 2024. Aidha, amesema mkakati huo wa nishati safi ya kupikia unaotekelezwa na Serikali ya Awamu Sita una lengo mahususi la kuboresha maisha ya wananchi kwa kuhakikisha ifikapo 2034 asilimia themanini (80) ya watanz...