Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 19, 2026

DAWA NA VIFAA TIBA VYA MIL 822.8 VYAKAMATWA TABORA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora . MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Magharibi imefanya oparesheni maalumu na kufanikiwa kukamata dawa zenye thamani ya sh mil 822.8 zilizokuwa zinauzwa kinyume na utaratibu.   Hayo yamebainishwa jana na Meneja wa TMDA Kanda ya Magharibi, Christopher Migoha alipokuwa akiongea na waandishi wa habari, ambapo alieleza kuwa jumla ya kilo 2,300 zenye thamani ya shilingi mil 822.8 zimekamatwa na kuteketezwa. Amefafanua kuwa dawa na vifaa tiba hivyo vimekamatwa katika oparesheni maalumu iliyofanyika katika hospitali, vituo vya afya, zahanati na maduka ya dawa baridi za binadamu na mifugo katika Wilaya zote. Migoha ameeleza kuwa dawa hizo haziruhusiwi kuuzwa katika maduka ya watu binafsi na ni kinyume cha sheria na kanuni ya 63 ya mwaka 2005 ya dawa zilizozuiliwa kuuzwa hadharani hususani katika maduka ya watu binafsi. Ameongeza kuwa katika operesheni hiyo walikagua jumla ya maduka 408 ya dawa, Hospital 16, vituo vya afya 17, zahanati 17, famas...

GOD MWANGA ATENGENEZA BARABARA 23 KWA GHARAMA ZAKE

Picha
  Na Mwandishi wetu, Moshi. MCHIMBAJI maarufu wa madini mbalimbali nchini God Mwanga amejitolea na kufanikisha ujenzi wa barabara tofauti 23 katika eneo la Mwika Kirueni, Wilayani Moshi Mkoani Kilimanjaro. Mchungaji mstaafu John Mlay ameyasema hayo wakati wa sherehe za kuukaribisha mwaka mpya wa 2026 zilizofanyika nyumbani kwa ukoo wa mzee Mathayo Mwanga katika eneo la Mwika Kirueni. Mchungaji Mlay ameeleza kwamba Mkurugenzi wa kampuni ya God Charity, Godlisten Mwanga amekuwa baraka kwa wakazi wa eneo hilo na kutengeneza barabara hizo kwa gharama zake mwenyewe. "Huyu baba amefanya jambo jema kwani ametumia magari na mitambo yake binafsi na kutengeneza barabara 23 kwa gharama zake mwenyewe," amesema Mchungaji Mlay. Amesema barabara hizo 23 zilikuwa na changamoto ya ubovu na hasa wakati mvua zikinyesha zinapitika kwa shida mno ila baada ya kutengenezwa hivi sasa hazina shida. "Hivi sasa barabara hizi zinapitika kwa urahisi mno baada ya God Mwanga kufanya kazi hiyo kubwa ya...