Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba 2, 2025

WAZIRI MAVUNDE AMPONGEZA RMO KASEZA

Picha
Na Mwandishi wetu, Mirerani  WAZIRI wa Madini Mhe Anthony Peter Mavunde, amempongeza Afisa madini mkazi (RMO) wa mkoa wa kimadini wa Mirerani, George Kaseza kwa namna anavyotekeleza wajibu wake ipasavyo, bila kulalamikiwa au kubagua wachimbaji. Waziri Mavunde ameeleza hayo wakati akizungumza na wadau wa madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, alipofanya ziara ya kutembelea machimbo ya madini ya Tomarini ya kijani eneo la Lemshuku na madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani. Amesema RMO Kaseza ni kiongozi mzoefu katika suala zima la eneo tengefu la Mirerani ndiyo sababu akateuliwa kuwa kiongozi wa hapo ambaye wadau wa madini pia wanamkubali kupitia utendaji kazi wake. "RMO Kaseza umekuwa mara nyingi ukiandika maandiko mengi ya eneo tengefu la Mirerani ndiyo sababu tukakuleta hapa sasa yake maandiko yako yafanye kuwa uhalisia ili yaonekane kwa vitendo," amesema Waziri Mavunde. Amewaasa wadau wa madini wa eneo hilo kumpa ushirikiano wa kutos...