REA KUIMARISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUPITIA MAJIKO BANIFU MKOANI MWANZA
Na Mwandishi Wetu, Mwanza. WAKALA wa Nishati Vijijini (REA) umemtambulisha rasmi mtoa huduma, kampuni ya Envotec Services Limited, kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mtanda, kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku kwa wananchi wa mkoa huo. Utambulisho huo ni sehemu ya juhudi za Serikali kupitia REA za kuendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini, kwa lengo la kuboresha afya za wananchi, kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa mazingira pamoja na kuhifadhi mazingira. Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mtanda, ameipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza na kusimamia miradi mbalimbali ya nishati yenye manufaa kwa wananchi, ikiwemo mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku. Amesema mradi huo ni muhimu kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kwani utasaidia kuongeza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa pamoja na kusaid...