Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 19, 2026

TUMUOMBEE RAIS, TULIOMBEE TAIFA-MASHILI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Nzega.  WATANZANIA wamehamasishwa kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aweze kupata utulivu wa kuliongoza Taifa la Tanzania kwa amani, upendo na mshikamano. Rai hiyo imetolewa leo Aprili 19, 2026 na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya MASHILI COMPANY LIMITED ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Uchenjuaji Dhahabu wa (Matinje Mining, Msilale Mining na Igurubi Mining) Ndg Peter Andrea Mashili aliposhiriki tamasha la Inland Festival lililoandaliwa na kanisa la Africa Inland Church Tanzania - AIC Wilayani Nzega mkoani Tabora. Mashili amesema kuwa Mhe Rais Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuifungua nchi na kuleta maendeleo hivyo ni jukumu la wananchi kuhakikisha wanamuombea ili aweze kuongoza kwa busara na mshikamano wa kitaifa. Pia Mashili amewataka viongozi wa dini na wananchi wote wa wilaya ya Nzega kumuombea Mbunge wa jimbo la Nzega Mjini Mhe Hussein Bashe ili aweze kuitumikia nafasi yake kwa ...

HAMISI KIM KOMANDO AWAPA COMPUTER MAKIBA SEKONDARI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Arumeru.  MDAU wa madini ya Tanzanite, Hamisi Kim Komando ametoa zawadi ya kompyuta shule ya sekondari Makiba ya Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kwa ajili ya matumizi ya masomo ya Tehama. Kim ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa bodi ya shule ya sekondari Makiba ameeleza hayo kwenye maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa shule hiyo mwaka 1996 na mahafali ya 15 ya kidato cha sita. Amesema anaiunga mkono shule hiyo kwa kununua kompyuta moja kwa ajili ya wanafunzi hao waboreshewe suala zima la Tehama. "Nawapongeza wanafunzi wote kwa kuhitimu kidato cha sita na ninawatakia kila la heri katika mtihani wenu mtakaofanya hivi karibuni," amesema Kim. Mkuu wa shule ya sekondari Makiba, Paul Kimaro amesema wameweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na changamoto ili wanafunzi wasome kidijitali kwa kutumia kompyuta. Kimaro amesema wanaendelea kutafuta wadau wa maendeleo, kuboresha usimamizi wa rasilimali zilizopo na kuhamasisha matumizi sahihi ya Tehama katika el...