Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi 29, 2026

MWENYEKITI MAREMA AWASIHI WACHIMBAJI KUSAIDIA WAATHIRIKA WA MAFURIKO

Picha
  Na mwandishi wetu, Mirerani.  MWENYEKITI wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) Elisha Nelson Mnyawi amewaomba wadau wa madini kujitolea na kuwasaidia waathirika wa mafuriko katika Tarafa ya Moipo. Mwenyekiti huyo wa MAREMA Mnyawi ameyasema hayo mji mdogo wa Mirerani, leo jumapili Machi 29,2026 wakati akikabidhi kwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mwalimu Fakii Raphael Lulandana vyakula na vifaa vya thamani ya shilingi milioni 22 vilivyotolewa na kampuni ya Permanent Mining LTD kwa ajili ya waathirika wa mafuriko katika Tarafa ya Moipo. Ameeleza kuwa japokuwa wachimbaji madini wamekuwa wakijitoa mara kwa mara kupitia hisani kwa jamii (CSR) wasiliache hilo likapita bila kuchangia chochote. Amesema wachimbaji mbalimbali ikiwemo Franone Mining, God Mwanga, Chusa Mining, California Camp, Bilionea Saniniu Laizer, Sunda Mining wamekuwa wakisaidia jamii wasaidie pia waathirika hao waliokumbwa na mafuriko. "Kupitia hadhara hii nampongeza Mkurugenzi wetu God Charity amba...

MTI MMOJA, ENEO AMBALO SIMBA HULITUMIA KWA HONEYMOON KRETA YA NGORONGORO.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Ngorongoro.  UNAWEZA kustaajabu lakini ukweli upo hivyo, ukitaka kuwaona simba wakiwa katika harakati za kuongeza familia fika katika  Kasoko ya Ngorongoro eneo la mti mmoja ambalo limezungukwa na vichaka, miti na nyasi za wastani. Eneo hili ni maarufu sana kwa waongoza utalii kutokana na makundi ya simba waliopo katika hifadhi hiyo kupenda kupumzika  na hasa wanapokuwa katika msimu wao wa kujamiina ama kutafuta watoto na kuongeza familia. Simba hupenda kujamiiana mara baada ya kushiba ambapo zoezi hilo linafanyika mda wowote mchana au usiku. Tofauti na Binadamu ambapo Kazi Ngumu hufanywa na wanaume, kwa Simba ni tofauti, kazi ya kutafuta chakula ama Mawindo kwa ajili ya msosi wa familia huongozwa na simba jike ambapo mara baada ya kuhisi njaa na tamaa ya kujamiina huamua kutafuta chakula ili kwanza kushiba halafu kuingia kwenye harakati ya kuongeza familia. Wakati wa mawindo simba huchagua chakula cha kushiba na hapa ina maana simba hahangaiki s...

TANZANIA YASHINDA TUZO YA KIMATAIFA YA UFADHILI WA MIUNDOMBINU.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Afrika Kusini.  SERIKALI kupitia Wizara ya Fedha imeendelea kung’ara kimataifa baada ya kushinda tuzo ya “Infrastructure Finance Deal of the Year 2026” zinazotolewa na Global Banking & Markets, kufuatia mafanikio ya upatikanaji wa mkopo wenye masharti nafuu wa dola za Marekani bilioni 1.78 kwa ajili kugharamia ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme (SGR) kwa kipande cha tatu na cha nne. Tuzo hiyo imepokelewa na Kaimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bw. Rished Bade, kwa niaba ya Wizara ya Fedha katika hafla ya utoaji Tuzo za Global Banking & Markets iliyofanyika jijini Cape Town, Afrika Kusini. Ushindi huo unatokana na mpango mahiri wa utafutaji ufadhili wa mradi huo mkubwa wa kimkakati, unaotarajiwa kuchochea ukuaji wa uchumi na kurahisisha usafirishaji nchini na Ukanda wa Maziwa Makuu, mkopouliopatikana kupitia ushirikiano kati ya taasisi za bima kutoka nchi za Sweden, Poland na Italy pamoja na Benki za Maendeleo za Kikanda, chini ya uratibu wa Benki ya St...