Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 14, 2026

CCM YASHITUKA KUHUSU MIKUTANO YA KUCHOCHEA MAAANDAMANO.

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kinazo taarifa zinazoashiria kuwepo kwa mikutano inayofanywa na baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambayo inadaiwa kuhusisha mipango ya kuhamasisha maandamano yenye uwezekano wa kuvuruga hali ya amani nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa CCM anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Kenani Kihongosi, alisema chama hicho kimeendelea kuwataka Watanzania kuzingatia umuhimu wa utulivu na mshikamano wa kitaifa. Kihongosi ameeleza kuwa CCM inaamini maendeleo endelevu hayawezi kupatikana iwapo kutakuwa na misukosuko ya kisiasa, akisisitiza kuwa tofauti za vyama zinapaswa kuishia kwenye majadiliano ya sera. Alisema chama hicho kinatoa tahadhari kwa wananchi kutoshawishika kushiriki katika matukio yanayoweza kusababisha machafuko, akibainisha kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa. “Taarifa tulizonazo zinaonyesha k...

WACHIMBAJI WATAKIWA KUJIUNGA WCF

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani.  WACHIMBAJI wa madini nchini wametakiwa kuwalipia wafanyakazi wao asilimia 0.5 ya mishahara yao ili kuwachangia kwenye mfuko wa fidia kwa wafanyakazi utakaowanufaisha pindi wakipata madhila kupitia mafao saba. Mwakilishi wa Meneja mkuu wa mfuko wa fidia kwa wafanyakazi (WCF) Naanjela Msangi ameeleza hayo akizungumza na viongozi wa wachimbaji madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. Msangi ameeleza kuwa endapo wamiliki wa migodi wakiwalipia wafanyakazi wao asilimia 0.5 ya mishahara yao kila mwezi watanufaika na mambo mengi ikiwemo kujikinga na kuzuia vihatarishi vya ajali. Amesema endapo wafanyakazi wakichangiwa watanufaika kwa kulipwa fidia katika sekta rasmi wanaopata ajali, ugonjwa ama kufariki dunia. "Katika kuteketeza jukumu hili WCF inatoa jumla ya mafao saba ambayo ni huduma ya matibabu, malipo ya ulemavu wa muda na wa kudumu na malipo kwa anayemhudumia mgonjwa," amesema Msangi. Ametaja mafao mengine ni ...