Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 12, 2026

UMIKIDO WASHIRIKI MKUTANO MKUU WA MWAKA WA VYOMBO VYA UTANGAZAJI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  UMOJA wa Vyombo vya Habari vya Mitandao ya Kijamii Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO) umeshiriki Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji nchini. Mkutano huo wa siku mbili unafanyika katika Ukumbi wa New Generation jijini Dodoma, ukianza leo Februari 12, 2026. Mkutano huo umeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Katika mkutano huo, mada na mafunzo mbalimbali yanawasilishwa kwa waandishi wa habari pamoja na wadau wa sekta ya utangazaji.  Aidha, kunafanyika mijadala mbalimbali inayolenga kujadili masuala muhimu yanayohusu maendeleo na uboreshaji wa vyombo vya utangazaji nchini. Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma.

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA ZALETA NEEMA IGUNGA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  SIKU 100 baada ya kuingia madarakani katika awamu ya pili ya uongozi wake,  Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta neema kwa wakazi wa Mji wa Igunga Mkoani hapa kwa kuwawezesha kupata huduma ya maji kwa masaa 24 kila siku. Akizungumza na gazeti hili jana, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Igunga (IGUWASA) Alex Ntonge ameeleza kuwa kazi nzuri iliyofanywa na Mheshimiwa Rais imemaliza changamoto za huduma ya maji. Amebainisha kuwa maboresho makubwa ya miundombinu na kupanuliwa kwa mradi wa maji ya Ziwa Victoria kumewezesha wakazi wote wa Mji huo na maeneo jirani kupata huduma ya maji safi na salama wakati wote, kwa masaa 24 kila siku. ‘Kazi nzuri iliyofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika siku 100 za kwanza tangu aingie Ofisini, imeleta neema, mabilioni aliyotuletea yameendelea kuboresha huduma ya maji na usafi wa mazingira Mji wote’, amesema. Mkurugenzi amefafanua kuwa zaidi ya asilimia 98 ya wakazi wote wa Mj...

GHAZALY AMPONGEZ WAZIRI MPYA WA VIJANA NA MICHEZO

Picha
Na Mwandishi Wetu, Misri.  MTAFITI wa Anthropolojia Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Afromedia, mpango wa uandishi wa habari na vyombo vya habari barani Afrika, pamoja na timu ya Afromedia, wanatoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Waziri Gohar Nabil kwa kuteuliwa kwake kuwa Waziri wa Vijana na Michezo, kufuatia kutolewa kwa amri ya rais na kuapishwa kwake rasmi. Katika taarifa yake, Ghazaly alieleza kuthamini kwa kina imani aliyopewa, akisisitiza kuwa hatua inayofuata inahitaji maono mapya na sera madhubuti za kuwawezesha vijana, kuendeleza vipaji vya michezo, na kuifanya michezo kuwa chombo muhimu cha maendeleo, kwa kuendana na mkakati wa taifa la Misri na dira ya Jamhuri Mpya. Ghazaly pia alibainisha umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa Kiafrika katika nyanja za vyombo vya habari, vijana na michezo, kwa lengo la kujenga madaraja kati ya mataifa, kuimarisha maadili ya pamoja, kugundua na kukuza vipaji vya vijana wa Afrika, kuangazia mifano chanya, kutangaza mipango ya pamoja, na kusu...

.MAIPAC YAWANOA WAANDISHI

Picha
  Na mwandishi wetu. Arusha.  TAAASI ya waandishi wa habari ya kusaidia jamii za pembezoni (MAIPAC) imetoa mafunzo kwa waandishi wa habari nchini, ya uandishi wakati wa migogoro ambao unazingatia usalama.wao na amani. Mafunzo hayo yameshirikisha waandishi wa habari kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Geita, Mara, Manyara, Mbeya na Arusha, yalidhaminiwa na shirika la wanahabari la Press Unlimited. Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi wa MAIPAC, Mussa Juma aliwataka wanahabari wanaokwenda kuripoti migogoro kuzingatia kuchukuwa tahadhari za kiusalama na.kutopendelea sehemu yoyote.  Juma amesema habari za upande mmoja ambazo hazizingatii maadili na maslahi mapana ya Umma zimekuwa zikisababisha migogoro katika jamii. Hata hivyo, amewataka wanahabari wakati wote wa kazi zao kuzingatia usalama wao,kufanya upembuzi yakinifu wa habari wananayotaka kuandika kabla ya kuandika na baada ya kuandika. "Tujuwe habari ina madhara gani,inafaida gani ,tusiwe na upande katika hiyo habari na...