Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi 28, 2026

DAKTARI HATIANI KUUZA SARUJI NA MATOFALI ZAHANATI SUKURO

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  MGANGA mfawidhi wa zahanati ya kijiji cha Sukuro kata ya Komolo wilayani Simanjiro mkoani Manyara, Dk Daud Ndagala ametiwa hatiani kwa ubadhirifu wa mifuko ya saruji na matofali ya kukarabati zahanati hiyo. Mahakama ya wilaya ya Simanjiro imemtia hatiani Dk Ndagala kupitia shauri la jinai namba 4344/2026 kwa makosa mawili ya uhujumu uchumi. Hakimu mkazi mkuu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Simanjiro Charles Uisso amesoma hukumu hiyo Machi 26,2026 na mwendesha mashtaka wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) kituo maalum cha Mirerani Gervas Sarakikiya. Hakimu Uisso ameieleza mahakama hiyo kuwa Dk Ndagala ametiwa hatiani kwa kufuja Sh1 milioni za mauzo ya mifuko 57 ya saruji ya kukarabati zahanati hiyo. Amesema pia, Dk Ndagala alichepusha tofali 220 zilizoandaliwa kwa ajili ya ukarabati huo kisha akaziuza Sh605,000 kwa mtu binafsi. Amesema mshtakiwa huyo amefanya makosa hayo akitumia nafasi yake ya mganga mfawidhi wa zahanati ya ...

MAMBO YALIYOJIFICHA KUHUSU HIFADHI YA TAIFA YA MILIMA UDZUNGWA

Picha
  1. Hifadhi ina njia mbalimbali za matembezi ya miguu na jumla ya Maporomoko ya maji 6 (Sanje, Sonjo, Njokamoni, Prince Benhard, Ichonde na Mwaya). 2. Vilele vikubwa vya  Milima (Luhomero mita 2,576  na Mwanihana mita 2,500 kutoka usawa wa bahari). 3. Kitovu cha Viumbe Adimu. Udzungwa ina viumbe wengi adimu ambao huwezi kuwapata mahala popote duniani. Spishi hizo ni pamoja na jamii mbili za primata (Ngolaga wa Sanje na Mbega wekundu wa Iringa), Spishi 2 za ndege (Kware wa Milima ya Udzungwa na “Rufous-winged Sunbird), Spishi 4 adimu za mimea ambapo moja wapo ni “Vernonia luhomeroensis”, Spishi 3 za vipepeo ambazo ni pamoja na “Charaxes lucyae mwanihanae”, Spishi ya Nyoka aitwaye “Red Snouted Wolf Snake na viumbe wengine wengi. 4. Baadhi ya Spishi nyingine adimu zinapatikana katika Milima ya Tao la Mashariki (Eastern Arc Mountains) baadhi ya spishi hizo  ni pamoja na Kinyonga Mfupi (Pygmy Chameleon).  #UdzungwaNountainsNationalPark #HikingParadise #tanzaniaparks...

UFAWAZA WAIPONGEZA DOREFA KWA USIMAMIZI NA UENDESHAJI SOKA DODOMA.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  UMOJA wa Wanamichezo wa zamani wa Mkoa wa  Dodoma (UFAWAZA) umekipongeza Chama cha Soka Mkoa wa Dodoma (DOREFA) chini ya Mwenyekiti Aden Mohammed kwa jinsi ambavyo kimekuwa  kikiendesha na kusimamia kwa weledi soka la mkoa wa Dodoma. Pongezi hizo zimetolewa leo Machi 28,2026 Jijini Dodoma na Mjumbe wa Ufawaza,Samson Mkotya wakati akizungumza katika Mkutano Mkuu wa DOREFA. Mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe wa Mkutano Mkuu kutoka Wilaya za Mkoa wa Dodoma pamoja na Vyama shiriki. Mkotya ambaye kitaaluma ni Mwalimu na Mwanasheria amesema DOREFA  imefanya mambo makubwa katika soka la Mkoa huo ikiwemo kuhakikisha soka linachezwa kuanzia katika ngazi za madaraja ya chini. "Kipekee naomba nikupongeze Mwenyekiti wetu (Aden Mohammed) tunajivunia wewe.Mkutano huu ni uthibitisho tosha mnatembea na Matukio  kwa kuhakikisha Mikutano ya kikatiba inafanyika hakika mnalitendea haki soka la Dodoma,"amesema Mkotya.

MKUTANO MKUU DOREFA WAPITISHA MPANGO KAZI KWA MWAKA 2026 - 2027

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dodoma (DOREFA) wamepitisha  Mpango kazi wa mwaka 2025-2026 wa Chama cha Soka Mkoani Dodoma. Awali kabla ya kuupitisha Mpango kazi huo,wajumbe hao walisomewa na Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dodoma CPA,Edwin Michael na kisha kwa kauli moja kuupitisha katika Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama hicho uliofanyika leo Machi 28,2026 Jijini Dodoma. Moja ya malengo ni kuhakikisha kunakuwa na ligi imara na yenye ushindani kwa vijana,kuendeleza mpira wa miguu kwa wanawake pamoja na kuendeleza ushirikiano na wadau wa Soka. "Mpango kazi huu,wa mwaka 2026-2027 unaweka msingi imara wa Maendeleo ya mpira wa miguu Mkoa wa Dodoma Kwa kushirikiana na wadau wote wa michezo na kuhakikisha Mkoa unakuwa na ushindani wa Kitaifa na Kimataifa,"amesema CPA Michael.

ADEN AAHIDI MAKUBWA DODOMA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma. MWENYEKITI wa Chama cha Soka Mkoa wa Dodoma (DOREFA) Aden Mohammed ameahidi makubwa zaidi kwa soka la Mkoa wa Dodoma ikiwemo kuweka mazingira rafiki kwa klabu zinazoutumia uwanja wa Jamhuri kama uwanja wa nyumbani. Aden ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF na Mjumbe wa Kanda namba 4 inayojumisha Mikoa ya Singida,Dodoma,Shinyanga na Simiyu amesema  wanafurahi  kwa jinsi ambayo Mkoa wa Dodoma umekuwa na timu nyingi za Ligi Kuu,Dodoma Jiji,Mtibwa Sugar na Tanzania Prisons. Amesema Dorefa itaendelea kuweka mazingira rafiki na wezeshi ili klabu hizo ziendelee kuutumia uwanja wa Jamhuri kama uwanja wa nyumbani kwa kuhakikisha zinafanya vizuri. "Niwaahidi wana Dodoma, Dorefa itaendelea kuhakikisha soka linachezwa kuanzia ngazi ya chini mpaka ya juu lengo vipaji vizidi kuonekana,"amesema Aden.