Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 26, 2026

NUKUU KUTOKA UN.

Picha
WAKATI dunia inaendelea kutumia fedha nyingi zaidi kwenye silaha na maandalizi ya vita, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anakumbusha kwamba, usalama wa kweli haujengwi kwa silaha, bali kwa imani, mazungumzo na utu wa binadamu. "Kupunguza silaha si jambo la kusubiri hadi amani ipatikane. Ni hatua ya kuzuia vita kabla havijaanza. Ni njia ya kujenga uaminifu kati ya mataifa. Ni kulinda maisha na mustakabali wa dunia yetu."  Sanamu ya Bunduki Iliyofungwa Fundo kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York City inaendelea kuwa ukumbusho kwamba amani huanza pale vurugu zinapokoma. #UN #habarikamilitv #USA #IRAN #URUSI # CHINA

SERIKALI YA RAIS SAMIA YATANGAZA KUNUNUA NDEGE MPYA NANE KWA MWAKA HUU

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  MSEMAJI Mkuu wa serikali ya Tanzania Bw. Gerson Msigwa leo Alhamisi Februari 26, 2026 amewaambia waandishi wa habari Mjini Dar Es Salaam kuwa serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kwa mwaka huu imepanga kununua ndege mpya nne kati ya nane walizopanga kununua ili kuongeza fursa kwa watanzania katika masoko ya kikanda na Kimataifa pamoja na kusisimua uchumi na Utalii wa Tanzania kama ilivyoahidiwa katika Kampeni za uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Akizungumza na waandishi wa habari kwenye Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere Dar Es Salaam, Msigwa amesema  ndege zitakazonunuliwa ni aina ya Bombardier Q400 kama sehemu ya utekelezaji wa mpango wa serikali katika kuimarisha mtandao wa huduma za usafiri wa anga ili kuwa kichocheo muhimu cha Utalii, biashara na usafiri. "Mimi nipo hapa kuwahakikishia kwamba katika lengo hili tumepata mafanikio makubwa, shirika letu sasa hivi tumepata mafanikio makubwa ambapo tumeanza kutajwa kama Shirika...

SERIKALI YATENGA BILIONI 5 KUFADHILI UZAMIVI DATA SCIENCE NA AI KUPITIA SAMIA SCHOLARSHIP

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  Serikali imetenga Shilingi bilioni 5 kufadhili wanafunzi 20 wa Shahada ya Uzamili katika fani za Sayansi Takwimu (Data Science), Akili Unde (Artificial Intelligence) na Sayansi Shirikishi kupitia mpango wa Samia Scholarship Extended (SSE DS/AI+), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa taifa kuimarisha rasilimali watu katika teknolojia za kisasa. Wanafunzi 10 tayari wameanza masomo yao katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST), huku wengine 10 wakitarajiwa kuanza katika Indian Institute of Technology Zanzibar. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, alisema mpango huo maalum wa ufadhili wa uzamili umeanzishwa kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya taifa katika maeneo ya teknolojia, ubunifu na uchambuzi wa takwimu. “Vyuo tunavyopeleka wanafunzi wa Samia Scholarship AI/DS+ vinatoa fursa ya mafunzo kwa vitendo katika makampuni makubwa ya teknolojia na vinaendelea kud...

MGODI WA ITRACOM WACHANGIA SHILINGI BILIONI 1.29 MAPATO YA SERIKALI MANYARA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Manyara.  MGODI wa Itracom Fertilizer Limited unaojihusisha na uchimbaji na uchakataji wa madini ya phosphate uliopo  katika eneo la Vilima Vitatu, Wilayani Babati mkoani Manyara, umechangia Shilingi Bilioni 1.29 katika mapato ya Serikali tangu kuanza kwa shughuli zake mwaka 2023. Hayo yamebainishwa na Mjiolojia, Waziri Mkupe, akizungumza kwa niaba ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Manyara, Godfrey Nyanda, ambapo amesema mapato hayo yametokana na mrabaha na ada ya ukaguzi wa madini. Amesema tangu kuanza kwa uzalishaji, mgodi huo umezalisha jumla ya tani 69,929 za madini ya phosphate zenye thamani ya Shilingi Bilioni 36.99, ambazo zimeuzwa katika soko la ndani na nje ya nchi, hususan Nala mkoani Dodoma na nchini Burundi. Kwa mujibu wa Mkupe, mchango huo umeimarisha ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali na kuchochea maendeleo ya jamii inayozunguka mgodi kupitia utekelezaji wa miradi ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR). Ameeleza kuwa tangu kuanza kwa shughuli zak...

MANISPAA TABORA YATOA TUZO KWA WADAU WA MAENDELEO

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora HALMASHAURI ya Manispaa Tabora imetoa tuzo maalumu kwa wadau zaidi ya 10 ambao wamekuwa mstari wa mbele kuunga mkono juhudi za maendeleo zinazofanywa na halmashauri hiyo ikiwemo kuchangia shughuli za kitaifa. Akikabidhi tuzo hizo jana kwenye kikao cha madiwani Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Ghullam Hussein Remtullah amempongeza Mkurugenzi Mtendaji Dkt John Pima kwa kuandaa tuzo hizo. Ameeleza kuwa tuzo hizo ni muhimu sana kwa kuwa zinadumisha ushirikiano na mahusiano mazuri na wananchi wanaojitolea kuchangia shughuli za maendeleo ikiwemo matukio makubwa ya kitaifa yanayofanyika katika manispaa hiyo. ‘Hawa tunaowapa tuzo leo ni wakulima, wafanyabiashara na wafugaji ambao wamekuwa wakijitolea kwa hali na mali kuishika mkono halmashauri ili kufanikisha mambo mbalimbali, walitoa chakula, fedha na mifugo’, amesema. Mstahiki Meya amebainisha kuwa manispaa inatambua na kuthamini mchango wao ndiyo maana leo wamekabidhiwa tuzo hizo, aliwaomba kuendele...