Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 18, 2026

MOKIA OLE MREFU AWATAKIA KILA LA HERI MAKIBA SEKONDARI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Arumeru.  MWENYEKITI wa chama cha wafanyabishara wa madini Mkoa wa Manyara na kurugenzi ya Habari na Mawasiliano wa chama cha wafanyabishara wa madini Taifa (CHAMMATA) Mokia Ole Mrefu, amewajengea uwezo na kuwapa moyo wanafunzi wa kidato cha sita wa shule ya sekondari Makiba Wilayani Arumeru Mkoani Arusha, wanaotarajia kufanya mtihani wao wa kuhitimu hivi karibuni. Ole Mrefu amezungumza na wanafunzi hao kwenye maadhimisho ya miaka 30 tangu shule hiyo ianzishwe na mahafali ya 15 ya kidato cha sita kwa kuwatakia kila la heri katika mtihani wao wa kuhitimu. 'Hongereni sana vijana wetu jasiri wa kidato cha sita mnaojiandaa kuhitimu, leo nasimama kuwapa moyo na kuwakumbusha jambo moja muhimu: mmefika hapa si kwa bahati, bali kwa juhudi, nidhamu, na uvumilivu wenu," amesema Ole Mrefu . Ameeleza kwamba safari waliyoipitia imekuwa na changamoto nyingi, masomo magumu, mitihani ya majaribio, na nyakati za kuchoka, lakini bado mmesimama imara, hiyo peke yake ni ushin...

WITO WATOLEWA KUIMARISHA UDHIBITI WA MAGONJWA YA MAZINGIRA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Morogoro.  SERIKALI imetoa wito wa kuimarisha ushirikiano kati ya sekta mbalimbali ili kudhibiti magonjwa yanayotokana na mazingira, hatua inayolenga kulinda afya ya jamii na kuzuia milipuko ya magonjwa. Rai hiyo imetolewa Aprili 18, 2026, mkoani Morogoro katika kikao cha kuandaa mwongozo wa ufuatiliaji wa viashiria vya mazingira na Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Dkt. Otilia Gowelle,  Dkt. Gowelle amesema sekta zinazopaswa kushirikiana kuwa ni pamoja na afya ya mazingira, maji, mamlaka za serikali za mitaa, taasisi za utafiti, wadau wa maendeleo na mashirika yasiyo ya kiserikali. “Ubunifu, maelewano na ushirikiano ni nguzo muhimu katika kuilinda nchi dhidi ya magonjwa yatokanayo na mazingira hivyo wajibu wetu kuhakikisha mwongozo huu unatumika kuleta mabadiliko chanya ya afya ya jamii” amesema Dkt. Gowelle. Gowelle, amepongeza timu ya wataalamu kwa juhudi za kukusanya na kuandaa maarifa yao katika mwongozo unaozingatia sera zilizopo, akibainisha kuwa ...

HONGERA FRANONE MINING UJENZI ZAHANATI MIGODINI

Picha
  Na mwandishi wetu, Mirerani  MACHIMBO ya madini ya Tanzanite, Mji mdogo wa Mirerani, Wilayani Simanjiro, Mkoani Manyara, ina migodi 2,000 yenye leseni hai 145 na watu 12,000 wenye kuingia na kutoka kila siku wakiwemo 5,000 wanaolala eneo hilo, haina hospitali wala kituo cha afya, hata zahanati. Wataalamu watetezi wa haki za binadamu wanaeleza kuwa haki kubwa kuliko zote ni haki ya kuishi kwani ukiwa hai utaweza kupata haki nyingine zilizobaki hivyo ili uishi inapaswa miundombinu ya afya nayo iwepo. Wataalamu hao wanaeleza kwamba uhai ni muhimu katika maisha ya binadamu ndiyo sababu mtu akiugua au akipata ajali anapelekwa hospitalini, kituo cha afya au zahanati, kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Mkuu wa wilaya ya Simanjiro Fakii Lulandana hivi karibuni alifanya ziara kwenye machimbo ya madini ya Tanzanite na kukagua zahanati inayojengwa na kampuni ya Franone Mining waliojitolea kwa ajili ya kutoa matibabu kwa wachimbaji madini. Kwa ujenzi wa zahanati hiyo katika migodi ya madin...