Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 8, 2026

WAZIRI AWESO APELEKA NEEMA URAMBO

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. WAKAZI wa Wilaya ya Urambo Mkoani Tabora wamelipuka kwa shangwe na furaha baada ya Waziri wa Maji Jumaa Aweso kuagiza maji ya ziwa Victoria yafikishwe katika Wilaya hiyo ndani ya wiki tatu kuanzia sasa. Waziri ametoa agizo hilo jana alipokuwa akizungumza na mamia ya wakazi wa Wilaya hiyo katika Kata ya Muungano baada ya kutembelea na kukagua Mradi wa Maji wa Miji 28 unaotekelezwa na serikali ya awamu ya sita katika Wilaya tatu za Mkoa huo. Amesema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imetoa shilingi bilioni 143 ili kuleta maji ya uhakika ya ziwa Viktoria katika Wilaya za Kaliua, Urambo na Sikonge ambazo zinashida kubwa ya maji. ‘Mradi huu utekelezaji wake unaenda vizuri sana, ujenzi wa tanki kubwa la kupokelea maji tayari umekamilika, na nimeambiwa kuwa kipande kilichobakia hakizidi hata kilometa moja maji yatakuwa yamefika hapa Urambo’, ameeleza. ‘Nitawaongezea shilingi milioni 500 za mabomba ili kazi hii ifanyike ha...

WAANDISHI KUCHUNGUZA SHOROBA NA MABADILIKO TABIA NCHI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Arusha. Waandishi wa habari kanda ya kaskazini na kati, wamekubaliana kuandika uchunguzi wa uvamizi njia za wanyamapori (Shoroba) na athari za mabadiliko tabia nchi nchini. Mapito mengi ya wanyama nchini ikiwepo ya Kwakuchinja yaliyopo katikati ya  hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Manyara yanaendelea kuvamiwa na watu ajili ya shughuli za kibiaadamu na kuathiri wanyamapori kuhama na biolojia yao. Mabadiliko ya tabia nchi yanayochangiwa na uharibifu wa mazingira yameanza kusababisha kumezwa ardhi maeneo kadhaa ikiwepo eneo la pangaji mkoani Tanga na ukame maeneo mengi nchini ikiwepo ya jamii za asili na kupungua barafu mlima Kilimanjaro . Maamuzi ya kufanya uchunguzi hao yalifikiwa  katika mafunzo ya uandishi wa habari za mazingira yaliyoandaliwa na mtandao wa watetezi wa haki za binaadamu(THRDC) kwa kushirikiana na Taasisi ya waandishi wa habari ya kusaidia jamii za asili (MAIPAC) kwa udhamini wa shirika la Umoja wa Mataifa la UNESCO. Akizungumza katik...

WADAU WA BIASHARA WAELIMISHWA NAMNA YA KUPATA HAKI KUPITIA BARAZA LA USHINDANI

Picha
Na.Mwandishi Wetu- Mwanza. BARAZA  la Ushindani wa Soko (FCT)  limetoa mafunzo ya kuwajengea uwezo wafanyabiashara jijini Mwanza, yakilenga kuwaongezea uelewa kuhusu masuala ya ushindani wa soko pamoja na taratibu za kupata haki katika shughuli za kibiashara. Mafunzo hayo yaliwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya biashara, ambapo waliipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa juhudi zake za kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kupitia uwepo wa chombo huru cha kusimamia na kudhibiti ushindani wa soko. Akifungua semina hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Bw. Balandya Elikana, alisema kuwa mafunzo hayo ni muhimu kwa wadau wa sekta ya biashara kwani yanawawezesha kuelewa kwa kina majukumu ya Baraza la Ushindani pamoja na umuhimu wa mshikamano katika utekelezaji wa sheria za ushindani. “Kupitia semina hii, wadau watapata uelewa mpana kuhusu Bara...