Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba 9, 2025

WAZIRI MAVUNDE AZINDUA RASMI SHUGHULI ZA UJENZI WA MGODI MKUBWA WA MADINI YA KINYWE MAHENGE

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mahenge -Morogoro.  WAZIRI wa Madini, Mhe. Anthony Peter Mavunde (MB), amezindua rasmi shughuli za ujenzi wa mgodi wa madini ya graphite wa Kinywe, unaotekelezwa na kampuni ya Faru Graphite Corporation kwa ubia kati ya Serikali ya Tanzania (hisa 16%) na Black Rock Mining Limited (hisa 84%) ikiwa ni hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya sekta ya madini nchini. Akizungumza katika hafla iliyofanyika leo tarehe 9 Oktoba 2025 katika eneo la Mahenge, Wilaya ya Ulanga, Mkoa wa Morogoro, Mhe. Mavunde amesema uzinduzi huo ni ishara ya kasi mpya ya uendelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati katika Sekta ya Madini, kutokana na maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.  “Mradi huu si uchimbaji wa rasilimali pekee, bali ni injini ya maendeleo itakayochochea ukuaji wa viwanda, biashara, ajira, na ustawi wa jamii katika eneo la Mahenge kwa ujumla” amesema Waziri Mavunde. Kwa mujibu wa Waziri Mavunde, mradi wa Mahenge unatarajiwa kugharimu takriban...

WANANCHI ITILIMA WAIPONGEZA SERIKALI KWA KUUNDA MFUMO WA MALIPO YA KIFUTA JASHO /MACHOZI

Picha
  Na Mwandishi Wetu- Itilima. Wananchi wa vijiji vya Nyantugutu, Lung'wa na Nding'ho vya Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu wameipongeza Serikali kwa kuunda na kuboresha   mfumo wa ukusanyaji  wa taarifa  za wanyamapori  wakali na waharibifu (Problem animal information  system- PAIS) ambao umerahisisha malipo ya kifuta jasho (machozi) pindi madhara ya wanyamapori wakali na waharibifu yanapotokea kwa wananchi. Hayo yamesemwa na Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ndi'hgo , Bi. Salome Kambona katika mkutano wa hadhara wa kuelimisha wananchi namna ya kukabiliana na changamoto za wanyamapori wakali na waharibifu uliofanyika kijiji cha Ndi'hgo ,Wilaya ya Itilima leo Oktoba 9, 2025. "Tunaishukuru Serikali kwa mfumo huu ambao ndani ya siku saba mwananchi atatakiwa awe ametoa taarifa ya madhara yaliyotokana na mnyamapori ili aweze kulipwa" amesema Bi.Salome. Naye, Mkazi wa Kijiji cha Nyantugutu, Bw. Mosses Saguda amesema mfumo wa PAIS umepunguza urasimu na usumbufu wa m...

KIWANDA CHA KUSAFISHA DHAHABU CHUNYA CHAKAMILIKA , SERIKALI YATIMIZA AHADI

Picha
  ***Ni kupitia Kampuni ya Kitanzania ya Giant Equipment and Mashine’s Limited* *Kina uwezo wa Kusafisha kilo 20 za Dhahabu kwa Siku* *Mkuu wa Wilaya  Alhaji Batenga asema Chunya itajitosheleza kwenye mnyororo wa Madini* Na Mwandishi Wetu, Chunya. CHUNYA imepiga hatua kubwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa Kiwanda cha Kusafisha Dhahabu cha Giant Equipment and Machine’s Limited. Kiwanda hiki kina uwezo wa kusafisha kilo 20 za dhahabu kwa siku kwa usafi (purity) wa asilimia 99.9 na kiko mbioni kuanza uzalishaji rasmi, baada ya kukamilika kwa baadhi ya taratibu za Benki Kuu ya Tanzania (BoT) . Akizungumza katika mahojiano maalum na timu ya Madini Diary kutoka Wizara ya Madini, Meneja Uendeshaji wa Kampuni hiyo Hassan Pazi amesema tayari majaribio ya kusafisha dhahabu kiwandani hapo yamefanyika kwa awamu tatu tofauti na zote zimetoa matokeo ya kiwango cha kusafisha hadi asilimia 99.9, jambo linaloashiria kuwa dhahabu inayosafishwa na kiwanda hicho inakidhi vigezo vya kununuliwa n...