Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 26, 2026

SERIKALI YAZINDUA MFUMO "ONGEA NA WAZIRI, MWANACHI KUPEWA SAUTI YA MOJA KWA MOJA SEKTA YA AFYA

Picha
  Na WAF, Arusha. SERIKAL imetangaza mwanzo wa enzi mpya ya uwazi, uwajibikaji na ushirikishwaji wa wananchi katika sekta ya afya baada ya kuzindua rasmi kwa mfumo wa kidijitali wa “Ongea na Waziri wa Afya” unaomuwezesha mwananchi kuwasiliana moja kwa moja na Wizara ya Afya saa 24 kwa siku. Hayo yamesemwa na Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati wa  hafla ya uzinduzi iliyofanyika leo Januari 26,2026 jijini Arusha. Waziri wa Afya, Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, amesema mfumo huo ni utekelezaji wa vitendo wa dhamira ya Serikali ya kuisogeza huduma ya afya karibu na mwananchi na kuhakikisha sauti ya wananchi inatumika kama dira ya maboresho ya huduma. “Mfumo wa "Ongea na Waziri wa Afya" unatuma ujumbe ulio wazi kuwa sauti ya mwananchi si ya pembeni, bali ndiyo msingi wa maamuzi ya Serikali katika kuboresha huduma za afya,” amesema Waziri Mchengerwa. Amefafanua kuwa uzinduzi wa mfumo huo ni mapinduzi makubwa katika sekta ya afya kwa kuwa unajenga utamaduni mpya wa uongozi unaosiki...

HABARI PICHA

Picha
WAZIRI wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, leo Januari 26, 2026 amefanya kikao kazi na Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) chenye lengo la kujadili mikakati ya kuimarisha na kuendeleza utendaji wa wakala huo. Kikao hicho kimefanyika katika Ofisi za Wizara ya Nishati, Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesm Mramba, Mwenyekiti wa Bodi ya PBPA, Dkt. Lutengano Mwakahesya, Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon, pamoja na Wajumbe wa Bodi na Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati.

WIZARA YA MADINI YAJENGA MAABARA KUBWA YA KISASA DODOMA

Picha
  Na Hamida Ramadhan, Dodoma. WIZARA  ya Madini imetangaza ujenzi wa Maabara kubwa ya kisasa katika eneo la Nala, mkoani Dodoma, kwa lengo la kusaidia upimaji na utoaji wa taarifa sahihi za sampuli za madini. Maabara hiyo inatarajiwa kuwa kitovu cha utoaji wa huduma za madini kusini mwa Jangwa la Sahara. Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema hayo leo Januari 26,2026 jijini Dodoma wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa Siku 100 za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kipindi cha pili cha Awamu ya Sita ya Serikali. Amesema kuwa ujenzi wa maabara hiyo utaleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa Tanzania na nchi jirani, sambamba na kuwajengea uwezo wataalamu wa ndani.  Aidha, Wizara imeingia makubaliano na GST ili taasisi hiyo iwe kitovu cha utoaji huduma za maabara kusini mwa Jangwa la Sahara. Katika kuongeza thamani ya madini, Waziri Mavunde amebainisha kuwa Wizara inaendelea kwa kasi na ujenzi wa viwanda vya kuongeza thamani, ambapo hadi sa...

SERIKALI YASAJILI ZAIDI YA WAFABIASHARA NDOGONDOGO 119,000 NCHINI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dodoma. SERIKALI kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imesajili jumla ya wafanyabiashara ndogondogo 119,595 katika Mfumo wa Usimamizi na Usajili wa Wafanyabiashara Ndogondogo (WBNMIS), hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kunufaika na fursa mbalimbali za maendeleo. Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa wizara hiyo, Mheshimiwa Dorothy Gwajima, amesema mafanikio hayo yamepatikana katika kipindi cha siku 100 za utekelezaji wa ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambapo Serikali imejikita katika urasimishaji wa wafanyabiashara, utoaji wa mikopo nafuu na uwezeshaji wa makundi maalum. "Kati ya waliosajiliwa wanawake ni 73,341 na wanaume 46,254, huku makundi yaliyosajiliwa yakijumuisha machinga 103,102, mama na baba lishe 12,384 pamoja na waendesha bodaboda na bajaji 4,109," Amesema Waziri Gwajima. Ameeleza kuwa katika ...