Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 14, 2026

URAMBO WAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI

Picha
Na Allan Kitwe, Urambo. HALMASHAURI ya Wilaya ya Urambo Mkoani Tabora imefungua milango kwa wawekezaji wa ndani na nje kuja kuwekeza katika sekta mbalimbali, kwa kuanzia wametenga eneo la ardhi lenye ukubwa wa hekari 72 kwa ajili ya kazi hiyo. Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Grace Quintine alipokuwa akitoa taarifa ya maendeleo ya halmashauri katika kikao cha baraza la madiwani. Amesema kuwa halmashauri hiyo ni miongoni mwa halmashauri zenye mazingira bora ya uwekezaji na ardhi nzuri inayofaa kwa shughuli za kiuchumi ikiwemo kilimo cha mazao mbalimbali ya chakula na biashara. Amedokeza kuwa maboresho makubwa ya miundombinu ya huduma za kijamii ambayo yameendelea kufanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ni kivutio muhimu kwa wawekezaji. Guintine amefafanua kuwa Urambo ni mahali salama kwa uwekezaji na kwa  mwaka huu wa fedha wameratibu maeneo maalumu yanayofaa kwa uwekezaji na kutenga eneo lenye ukubwa w...

WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUZINGATIA KINGA NA TAHADHARI YA MAJANGA YA MOTO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Morogoro. WATUMISHI wa umma wametakiwa kutumia kikamilifu maarifa wanayoyapata katika kusimamia na kutekeleza kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto katika majengo na miradi yote ya serikali Wito huo umetolewa na  Dkt. James Henry Kilabuko akizungumza kwa niaba ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Wenye Ulemavu) wakati wa semina ya usimamizi wa kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto iliyowakutanisha Wakurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Taasisi za umma  Amesema changamoto ya ukosefu wa fedha kwa ajili ya ununuzi na ukarabati wa miundombinu ya kujikinga dhidi ya moto haipaswi kuwa kikwazo kwa watumishi wa umma kusubiri bila kuchukua hatua, bali watumie ipasavyo fursa na rasilimali zilizopo kujilinda wao wenyewe pamoja na kulinda mali za serikali. Ameongeza kuwa maandalizi, tahadhari na ufuatiliaji wa mara kwa mara ni nguzo muhimu katika kupunguza athari zinazotokana na majanga ya moto, akisisitiza ku...