Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 12, 2026

SERIKALI YAONYA WATAALAMU WA ARDHI WASIO WAADILIFU

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora SERIKALI imewataka watumishi wa sekta ya ardhi nchini kufanya kazi kwa weledi na uadilifu ili kuhakikisha migogoro ya ardhi iliyopo katika maeneo yao inatatuliwa kwa wakati ili kuepusha malalamiko ya wananchi. Onyo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Kaspar Kaspar Mmuya alipokuwa akiongea na watumishi wa sekta hiyo kutoka taasisi mbalimbali za umma Mkoani hapa. Ameeleza kuwa ni jukumu la wataalamu wa sekta hii kuhakikisha kero na migogoro yoyote inayohusiana na masuala ya ardhi inashughulikiwa ipasavyo na kwa wakati ili wananchi wapate haki zao. ‘Ninyi ni wawakilishi wa Mheshimiwa Rais katika sekta hii, onyesheni weledi wenu, fanyeni kazi kwa uadilifu mkubwa, kuweni na maadili mema, tendeni haki kwa wananchi wote ili wawaamini, wengi wenu mnaitwa wapiga dili’, amesema. Ameonya kuwa serikali haitamvumilia mtumishi yeyote wa sekta hii anayeendekeza vitendo vya upigaji dili badala ya kutekeleza wajibu wake kwa kuzingatia she...

IGEMBENSABO INAWATAKIA WANACHAMA WAKE WOTE HERI YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Picha
 

WALIMU SIMANJIRO WAJENGEWA UWEZO SIS

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro WAKUU wa shule za sekondari na msingi wilayani Simanjiro mkoani Manyara, wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule kutokana na kasi ya ukuaji na kuongezeka kwa matumizi ya sayansi na teknolojia ulimwenguni. Wakuu wa shule 23 za sekondari, 110 wa msingi wa shule za serikali na binafsi wamejengewa uwezo wa kuandaa taarifa za shule ili kurahisisha utoaji na upatikanaji wa wake kupitia serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Elimu.  Afisa elimu ya awali na msingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro, Darius Daudi Limandola amesema walimu hao wamepata mafunzo hayo ya uandaaji wa taarifa za shule kwenye vituo vitatu vya Orkesumet, Terrat na Mirerani. Limandola ameeleza kwamba mafunzo hayo ya mfumo wa utoaji wa taarifa za kielimu kupitia mfumo wa kidigitali (School Information System) una lengo la kurahisisha utoaji na upatikanaji wa taarifa za shule husika kwa wakati. Ameeleza kwamba mfumo huo unafanyak...