Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba 27, 2025

VIONGOZI WA DINI SINGIDA NA DODOMA WAHIMIZA VIJANA KULINDA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma. VIONGOZI wa Dini kutoka mikoa ya Singida na Dodoma wamewataka vijana kuepuka vishawishi vya vurugu na mifarakano ya kisiasa, wakisisitiza kuwa kulinda amani ni jukumu la kila Mtanzania kadri Taifa linavyoelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika wiki ijayo. Wito huo umetolewa leo jijini Dodoma katika kongamano la viongozi wa dini mbalimbali kutoka Kanda ya Kati, lililolenga kuliombea Taifa amani na utulivu kuelekea uchaguzi huo. Akizungumza katika kongamano hilo, Askofu Evance Chande wa Kanisa la Carmel Assemblies of God amesema vijana wanapaswa kutumia nguvu zao katika kujenga Taifa badala ya kushiriki katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha usalama wa nchi. “Tunapaswa kuikumbatia amani kama tunavyokumbatia imani zetu. Uchaguzi ukipita, Tanzania inabaki kuwa moja. Tusikubali kugawanywa kwa misingi ya kisiasa,” amesema Askofu Chande. Kwa upande wake, Sheikh Mustapha Rajab, Sheikh wa Mkoa wa Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati ...

MUNDE TAMBWE AENDELEA KUHAMASISHA USHINDI WA CCM SKON

Picha
  Na Hamida Ramadhani. MJUMBE wa NEC na aliyekuwa mtia nia wa ubunge Jimbo la Skonge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Munde Tambwe, ameendelea kujikita katika jimbo hilo akihamasisha wananchi kuichagua CCM katika uchaguzi ujao. Amesema sababu kuu ya kuichagua CCM ni mafanikio makubwa yaliyopatikana chini ya uongozi wake, ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya, shule, na miundombinu ya barabara, pamoja na uwezeshaji wa wananchi katika sekta ya kilimo. Munde amewataka wananchi waendelee kuiamini CCM kama chama kinachotekeleza ahadi zake na kuboresha maisha ya Watanzania.