Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba 20, 2025

FCC YANG’ARA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA WATAALAMU WA MANUNUZI NA UGAVI

Picha
Na.Mwandishi, Wetu. TUME ya Ushindani (FCC) imetunukiwa tuzo maalum ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Manunuzi na Ugavi nchini. Tuzo hiyo imekabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mshamu Munde, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, na kupokelewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano cha FCC, Bi. Roberta Feruzi. Hafla ya utoaji wa tuzo hiyo ilifanyika katika Kongamano la 16 la Wataalamu wa Manunuzi na Ugavi, lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), jijini Arusha lililoandaliwa na Bodi ya Wataalamu na Mafundi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB). FCC imeshiriki kongamano hilo kama mdau muhimu wa sekta ya manunuzi na ugavi, ambapo iliwasilisha mada kuhusu umuhimu wa ushindani wa haki katika masuala ya manunuzi na ugavi, hususan katika kulinda mnyororo wa thamani. Kupitia kongamano hilo, Tume pia ilitoa elimu kwa wadau mbalimbali kuhusu majukumu na kazi zake, ikisisitiza nafasi yake katika kuhakikisha mazingira ya ushindani yanayochochea uwazi, ufanisi na ...

ELIMU YA USHINDANI YAONGEZA UWAZI KWA WAFANYABIASHARA MBEYA

Picha
Na.Mwandishi Wetu. BARAZA la Ushindani (FCT) jana Desemba 18, 2025, limeendesha semina ya elimu kwa wadau mkoani Mbeya kwa lengo la kuongeza uelewa kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa na Baraza hilo. Semina hiyo ilifanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya na kufunguliwa na Katibu Tawala Msaidizi – Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mkoa wa Mbeya, Bi Anna Mwambene, ambaye aliwahimiza wadau kutumia ipasavyo mifumo ya kisheria iliyopo na kuwa mabalozi wa kuitangaza huduma za Baraza la Ushindani. Bi Mwambene alisema uelewa wa sheria na taratibu za ushindani ni muhimu katika kukuza mazingira bora ya biashara na uwekezaji, akisisitiza umuhimu wa wadau kushiriki kikamilifu katika kulinda haki zao kwa kutumia mifumo rasmi iliyowekwa na Serikali. Katika semina hiyo, Baraza la Ushindani liliwapatia washiriki elimu kuhusu matumizi ya mfumo wa kidijitali wa kuwasilisha rufaa zinazotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani (FCC) pamoja na mamlaka mbalimbali za udhibiti, zikiwemo LATRA, E...

TAKA ZAWAKELA WAFANYABIASHARA SOKO LA SABASABA DODOMA

Picha
  Na Hamida Ramadhani, Dodoma. WAFANYABIASHARA  wa soko la matunda na mbogamboga Sabasaba jijini Dodoma wameliomba Jiji la Dodoma kuondoa takataka zilizojaa katika dampo lililopo ndani ya soko hilo, wakisema hali hiyo inahatarisha afya zao. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, watanyabiashara hao wamesema dampo hilo limejaa kupita kiasi na takataka kushindwa kuondolewa kwa wakati, hali inayosababisha harufu kali na mazingira machafu, jambo linalodaiwa kuchangia baadhi yao kuugua maradhi mbalimbali yakiwemo ya mfumo wa hewa. Paulina, maarufu kama Mama Kibibi, ni mmoja wa wafanyabiashara sokoni hapo. Anasema hali ya taka kujaa kwa muda mrefu imemletea matatizo ya kiafya, hali inayomfanya ashindwe kufanya shughuli zake ipasavyo. Kwa upande wake, Agaudence Temba, mfanyabiashara wa matunda katika soko hilo, ameuomba uongozi wa Jiji la Dodoma kukaa meza moja na wafanyabiashara ili kutafuta suluhisho la kudumu. Anapendekeza kuwepo kwa mchango wa shilingi mia mbili kwa siku kutoka kwa wa...

JAFO ARIDHISHWA NA UJENZI WA MABWENI NA MADARASA SHULE YA SEKONDARI DK. SELEMANI JAFO

Picha
Na.Mwandishi Wetu-KISARAWE. MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ameridhishwa na hatua iliyofikiwa katika ujenzi wa mabweni mawili na madarasa katika Shule ya Sekondari Dkt.Selemani Jafo, na kuhimiza Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe kuhakikisha mradi huo unakamilika mapema ili ifikapo Januari 2026 shule hiyo iweze kupokea wanafunzi wa bweni. Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo wilayani Kisarawe, Dkt. Jafo amesema ziara hiyo ni sehemu ya kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hususan katika sekta ya elimu. “Tumeendelea na ziara yetu ya kuhakikisha tunasukuma utekelezaji wa ilani wilayani Kisarawe, na eneo kubwa tulilolipa kipaumbele ni uimarishaji wa sekta ya elimu. Hapa Shule ya Sekondari Selemani Jafo kuna kazi kubwa inaendelea, ikiwemo ujenzi wa mabweni mawili na madarasa ili kuboresha mazingira ya utoaji wa elimu,” amesema. Dkt. Jafo amepongeza usimamizi wa mradi huo, akieleza kuwa ujenzi umefikia zaidi ya asil...