Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 13, 2026

SHULE ZOTE 18055 ZA MSINGI ZIPO TAYARI KUPOKEA WANAFUNZI- PROF. SHEMDOE

Picha
  Na OWM - TAMISEMI  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameridhishwa na maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi wa darasa la awali na la kwanza katika Shule ya Msingi Iyumbu jijini Dodoma, na kuuarifu umma kuwa maandalizi katika shule zote za msingi 18055 yamekamilika na zipo tayari kupokea wanafunzi kuanzia Januari 13, 2026. Prof. Shemdoe amesema, ameitembelea shule hiyo ya Msingi Iyumbu leo Januari 12, 2026, ili kujiridhisha na maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi wanaotarajiwa kuanza darasa la awali na la kwanza Januari 13, 2026 na amejionea mwenyewe kuwa maandalizi yamekamilika. “Tumeona maandalizi kwenye shule hii yamekamilika, kama ilivyo kwenye shule zote 18055 za msingi, hivyo natoa wito kwa wazazi wenye watoto walio na umri wa kuanza darasa la awali na la kwanza wawapeleke shuleni,” Prof. Shemdoe amesisitiza. Prof. Shemdoe amejionea madarasa ya awali mazuri ambayo yamejengwa kwa fedha za mapa...

SELWA AKAGUA MIRADI 19 YA ELIMU IGUNGA YENYE THAMANI YA BILIONI 3.39.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga. MKURUGENZI Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Selwa Hamid amefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi 19 ya Afya na Elimu yenye tahamani ya sh. 3.39 bilioni. Selwa amefanya ziara hiyo ya siku tatu mfululizo katika kata zilizopo kwenye majimbo ya Igunga na Manonga wilayani Igunga. Amesema kukamilika kwa miradi hiyo ni muendelezo wa kuendelea kutoa huduma na furaha kwa wananchi.