Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba 17, 2025

BAROZI WA NORWAY NCHINI TANZANIA AKUTANA NA WAANDISHI ZANZIBAR.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  MHE. Balozi wa Norway nchini Tanzania, Tone Tinnes, na ujumbe wake wamekutana na waandishi wa habari na content creators ili kusikia simulizi za mafanikio yao kupitia program ya SWIL. Kupitia mafunzo ya wanawake na uongozi, waandishi wamekuwa daraja muhimu la kusambaza habari, kuibua mijadala na kuhamasisha jamii kuhusu usawa wa kijinsia.

MTANDAOO WA MSHIKAMANO WA KIMATAIFA UMEANDAA SALUNI YA KITAMADUNI KUADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA MSHIKAMANO WA KUSINI MWA DUNIA.

Picha
  *"Mazungumzo ya Mshikamano wa Kimataifa" huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mshikamano wa Kusini mwa Dunia* Na Mwandishi Wetu, Egypt  KATIKA  kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Mshikamano wa Kusini, Mpango wa Mazungumzo ya Mshikamano wa Kimataifa unaosimamiwa na Mtandao wa Mshikamano wa Kimataifa umeanda saluni ya kitamaduni.  Saluni hiyo yenye mada: "Vyama vya Ushirika katika Kusini ya Duniani", sambamba na tamko la Umoja wa Mataifa la kutangaza mwaka 2025 kuwa mwaka wa vyama vya ushirika chini ya kauli mbiu: "Vyama vya Ushirika: Sauti ya Pamoja ya Kusini Duniani kuelekea Mustakabali Endelevu." Saluni hiyo imemkaribisha Dkt. Mohamed Abdel Hakim Ibrahim, Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Uchumi wa Kijamii na Ushirika katika Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, na mwandishi wa kitabu cha “Vyama vya Ushirika na Maswali ya Maendeleo”, kama mzungumzaji mkuu katika Saluni hiyo.  Pia Saluni hiyo ilihudhuriwa na Mtafiti Hassan Ghazaly, Mwanzilishi wa Mtandao wa Ms...

HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU YAPOKEA TUZO.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Manyara.  HALMASHAURI ya Wilaya ya Mbulu imepokea tuzo za pongezi kwenye kikao cha tathmini ya lishe ya Mkoa kilichofanyika 12/09/2025 katika ukumbi wa vikao kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa. Tuzo hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imeshika nafasi ya kwanza(1) kati ya Halmashauri saba Kimkoa kwenye usimamizi mzuri na upatikanaji wa bidhaa za afya.Pia Halmashauri imeingia kwenye kumi bora ya waliofanya vizuri Kitaifa kati ya Halmashauri 184 nchini. Pia Halmashauri imepokea tuzo ya mshindi wa pili(2) kimkoa kwa sababu ya utekelezaji wa mkataba wa lishe,ikiwa na asilimia 99.4. Halmashauri imepongezwa kwa kuongeza mapato katika kituo cha Afya Dongobesh kutoka Milioni 3 hadi kufikia Milioni 18 kwa Mwezi.