Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 5, 2026

RUWASA KIGOMA WAMWAGA PONGEZI KWA RAIS SAMIA

Picha
  Na Allan Kitwe, Kigoma.  WAKALA wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoani Kigoma wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia zaidi ya shilingi bilioni 79 za miradi ya maji. Pongezi hizo zimetolewa na Meneja wa Wakala huo Mkoani hapa Mhandisi Mathius Mwenda alipokuwa akiongea kwenye mahojiano maalumu na waandishi wa habari Ofisini kwake. Amesema kuwa RUWASA Kigoma ina kila sababu ya kuishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kufanikisha utekelezaji miradi mbalimbali ya maji katika Wilaya zote 7 za Mkoa huo hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa kero ya maji. Mhandisi Mwenda amebainisha kuwa kuanzia Machi 2021 hadi Februari 2026, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan alitenga zaidi ya shilingi bilioni 79 kwa ajili ya kutekeleza miradi 113 ya maji katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huo. Amedokeza kuwa kati ya kiasi hicho cha fedha, serikali ilitoa jumla ya shilingi bilioni 55.9 na wadau wakaiunga mkono kwa kutoa kiasi cha shiling...

ASKOFU MEIVUKIE AASA JAMII KUCHUKUA TAHADHARI

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora WAKRISTO na jamii kwa ujumla wameaswa kuchukua tahadhari na kumwomba Mungu ainue wapatanishi dhidi ya mataifa ya Marekani, Israel na Iran ili vita inayoendelea sasa baina yao imalizike kwa amani ili kuepusha athari kwa jamii. Wito huo umetolewa jana na Askofu Paul Meivukie wa Kanisa la TAG-Jimbo la Tabora Kati ambaye pia ni Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kitete Christian Centre (KCC) alipokuwa akitoa salamu za pasaka kwenye ibada kanisani hapo. Amesema kuwa athari za vita vinavyoendelea sasa katika mataifa hayo ni kubwa mno, na Tanzania sio kisiwa, haiwezi kujitegemea kwa kila kitu, hivyo ni muhimu sana kumwomba Mungu na kutumia vizuri chakula tulicho nacho. Huu sio wakati wa kulaumu viongozi bali kuwaombea ili Mwenyezi Mungu awaongoze na kuwapa hekima ya kutoa maamuzi sahihi ili kuepusha bei za bidhaa kupanda zaidi hali inayoweza kuleta shida kwa wananchi. ‘Sote tunafahamu vita inayoendelea baina ya Marekani, Israel na Iran, naomba tuendelee kuchukua taha...

AFISA USAFIRISHAJI SIMANJIRO KORTINI KWA WIZI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Simanjiro.  Afisa usafirishaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, Ismail Khalifan amefikishwa mahakamani kwa kosa la jinai la wizi wa shilingi 500,000 akiwa mtumishi wa umma. Afisa usafirishaji huyo Ismail amefikishwa kwenye mahakama ya wilaya ya Simanjiro na kusomewa shitaka hilo la wizi wa shilingi 500,000 fedha ambazo ni mali ya Halmashauri hiyo. Mwendesha mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa (TAKUKURU) Faustin Mushi amesoma shataka hilo Aprili mosi, 2026 mbele ya hakimu mkazi mkuu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Simanjiro Charles Uisso. Mushi amesema Ismail anashtakiwa kwa kosa la wizi akiwa mtumishi wa umma kinyume na kifungu cha 258 (1), 265 na 270 vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya  16 R:E 2023. Amesema Ismail anashitakiwa kwa kosa la wizi wa shilingi 500,000 alizopewa na mwajiri wake kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya magari ya halmashauri ya wilaya hiyo. Amesema katika kesi hiyo ya jinai namba 7118/2026...