Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 18, 2026

REA YAHIMIZA WANANCHI KUJIUNGA NA HUDUMA YA UMEME TANGA

Picha
Wananchi wapewa elimu ya kufanya maombi ya umeme, waaswa kutumia umeme kwa tija kujiletea maendeleo. Na Mwandishi Wetu, Tanga.  WAKALA wa nishati vijijini (REA) umepiga kambi Mkoani Tanga kwa ajili ya zoezi la uhamasishaji wananchi kujiunga na huduma ya umeme. Uhamasihaji huo umefanyika katika maeneo ya pembezoni mwa wilaya ya Tanga mjini kwenye maeneo ya sokoni ,vituo vya bodaboda pamoja na mikutano ya hadhara iliyofanyika maeneo ya ofisi za kata na mitaa  lengo kubwa likiwa ni kuwapa uelewa wananchi juu ya umuhimu wa kujiunga na huduma ya umeme. Akizungumza wakati wa uhamasishaji Afisa maendeleo ya jamii kutoka REA , ndugu Abdulrazack Mkomi alisema , Lengo la wakala kufika wilayani humo ni kuwafikia wananchi na kuzungumza nao juu ya umuhimu wa kutumia fursa ya upatikanaji wa huduma ya umeme ambayo ni nafuu sana na kuwahimiza kujiunga mapema na huduma hiyo ya umeme hasa wakati ambapo mkandarasi bado yupo eneo la mradi. Aidha Mkomi amesema, utekelezaji wa miradi hii ya umeme u...