Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 17, 2026

ASKARI WA TFS WAPONGEZWA KULINDA SHAMBA LA MITI SILAYO.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Chato WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb),amewapongeza askari wa uhifadhi kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanaofanya kazi katika Shamba la Miti Silayo, wilayani Chato, kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kulinda na kuhifadhi shamba hilo kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. Dkt. Kijaji ametoa pongezi hizo leo, Aprili 16, 2026, alipokuwa katika ziara ya kukagua shamba hilo, akibainisha kuwa mafanikio yaliyopatikana yametokana na ari ya kujituma, mshikamano na umoja wa askari hao katika kuhakikisha shamba linabaki katika hali bora na ya kuridhisha. “Niwapongeze sana askari wetu mnaofanya kazi nzuri sana huku uwandani. Kazi yenu ni njema mno, tunawapongeza sana. Na pongezi hizi hazitoki kwangu tu, bali zinatoka moja kwa moja kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amenituma kuwafikishia pongezi hizi,” amesema Dkt. Kijaji. Aidha, ameongeza kuwa kazi wanayoifanya askari hao ni muhimu sana ...