Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba 8, 2025

WANAOHAMASISHA MAANDAMANO MTANDAONI HAWAPO NCHINI NA HAWAITAKII MEMA TANZANIA.

Picha
Na Mwandishi Wetu. WANANCHI na Wapiga kura wa Tanzania wamesisitizwa kupuuza na kutokubali kuhadaika na watu na baadhi ya wanasiasa wanaohamasisha vurugu na maandamano Jumatano ya Oktoba 29, 2025 siku ya upigaji wa kura kwenye uchaguzi Mkuu wa Tanzania. Wananchi tuliozungumza nao akiwemo Shaban Maulid na Adrian Malikale wamewasihi wananchi kujifunza na kutathmini athari za vurugu na machafuko kwa jamii hasa kwa watoto, wanawake na wazee, wakiahidi kutoandamana na kusisitiza kufuatwa kwa taratibu na sheria zinazotambulika kisheria wakati wa zoezi la upigaji kura. "Ni muhimu sana kutokubali kushawishiwa au kudanganyika kwenda kuandamana kwa namna yoyote ile ifikapo Oktoba 29, 2025. Tujitokeze tupige kura, turudi nyumbani kuendelea na shughuli zetu kama mimi mama lishe nitakavyofanya. " amesema Bi. Zuhura Mohamed. Tayari serikali ya Tanzania kupitia kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewahakikishia watanzania wote utulivu, amani na usalama siku hiyo ya upigaji wa kura, wakihimiz...

RC SENYAMULE; "THAMANI YA ARDHI YAPAA,DODOMA SASA NI KITUO KIKUU CHA MAENDELEO NCHINI.

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma. MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amesema kuwa thamani ya ardhi katika jiji la Dodoma inaendelea kupanda kwa kasi kila siku, kutokana na mabadiliko makubwa ya kiuchumi, kijamii na kimiundombinu yanayoendelea kujitokeza katika mji huo ambao sasa ni makao makuu ya nchi. Akizungumza jijini Dodoma katika kikao na viongozi wa dini mbalimbali, Senyamule alisema kuwa mabadiliko ya Dodoma kutoka kuwa mji mdogo hadi kuwa jiji linaloongoza kwa kasi ya ukuaji yamefungua milango ya uwekezaji, ajira, na ustawi wa wananchi kwa ujumla. “Zamani ukisema unaishi Dodoma mtu anakushangaa, lakini leo hii Dodoma imekuwa ndoto ya kila Mtanzania. Kila mtu anatamani kuwa sehemu ya mabadiliko haya Ardhi ya Dodoma sasa ni dhahabu  thamani yake inapanda kila kukicha,” amesema Senyamule. Aidha, amebainisha kuwa serikali imeweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji na wananchi kwa kuhakikisha huduma muhimu kama maji safi na salama, umeme wa uhakika, barabara za lami, pamoja na ...

MGOMBEA UBUNGE KUPITIA CHAMA CHA WANANCHI (CUF) AUAWA KWA KUCHOMWA NA KITU CHENYE NCHA KALI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Siha -Kilimanjaro. Mgombea ubunge wa Jimbo la Siha kupitia Chama cha Wananchi (CUF) mkoani Kilimanjaro, Daudi Wilbard Ntuyehabi, ameuawa na wananchi baada ya kudaiwa kumchoma kisu mtu mmoja aitwaye Abdul Issah Mohamed.  Tukio hilo lilitokea usiku wa Oktoba 7, 2025 katika Kijiji cha Kilingi, wilayani Siha. Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa, tukio hilo lilitokea majira ya saa 1:30 usiku, ambapo marehemu Daudi anadaiwa kumchoma kisu tumboni Abdul Issah Mohamed na kumsababishia utumbo kutoka Nike.  Inadaiwa kuwa Abdul alikuwa anajaribu kuingilia ugomvi uliokuwa ukiendelea kati ya Daudi na kijana mwingine waliokuwa wakizozana kuhusu deni la fedha wakiwa kwenye baa ya pombe maarufu kama ‘grocery’. Baada ya tukio hilo, wananchi waliokuwepo eneo hilo walimshambulia Daudi hadi kusababisha kifo chake. Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi linawashikilia watu nane kwa tuhuma za kujichukulia sheria mkononi,Kamanda Maigwa ametaja majina y...