Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 10, 2026

WAKAZI USUNGA WAFURAHIA MRADI WA MAJI

Picha
  Na Allan Kitwe, Sikonge.  WAKAZI wa Kijiji Cha Usunga, Kata ya Usunga Wilayani Sikonge Mkoani Tabora wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea mradi wa maji safi na salama ya kunywa. Wametoa shukrani hizo kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 58 tangu kuanzishwa kwa Kijiji hicho zilizofanyika jana kwenye uwanja wa CCM (Centre) na kueleza bayana kuwa serikali imemaliza kilio chao cha muda mrefu. Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho James Mgulu ameeleza kuwa mradi wa maji katika Kijiji hicho umeleta neema, furaha na shangwe kwa wananchi kwa sababu familia zao zilikuwa zinapata shida sana kwa kukosa maji safi na salama. ‘Tuna kila sababu ya kuishukuru serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea mradi huu wa maji na miradi mingine ya maendeleo, wananchi sasa wana amani tele, na maisha yao yamekuwa bora zaidi’, ameeleza.  Ameongeza kuwa wanapoadhimisha sherehe hiyo kila mwaka wanalenga kudumisha mila, utamad...

MIUNDOMBINU CHUO CHA NYUKI TABORA YABORESHWA

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora.  CHUO Cha Ufugaji Nyuki (BTI) Tabora kimeendelea kuboresha miundombinu yake kwa kujenga jengo jipya la kisasa la mihadhara linalogharimu zaidi ya shilingi milioni 500, utekelezaji mradi huu umefikia zaidi ya asilimia 48. Hayo yameelezwa jana na Mkuu wa Chuo hicho Semu Daud alipokuwa akiongea na mwandishi wa gazeti hili ofisini kwake, ambapo ameeleza kuwa jengo hilo litaboresha ufundishaji wa wakufunzi na kutatua changamoto ya uhaba wa vyumba vya madarasa chuoni hapo. Amefafanua kuwa ujenzi wa jengo hilo unafadhiliwa na Mfuko wa Misitu Tanzania (TAFF) ambao wametoa kiasi cha shilingi milioni 500 sawa na asilimia 82 huku shilingi milioni 92 sawa na asilimia 20 zikitoka kwenye mfuko wa chuo. Ukumbi huo utakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 400 kwa wakati mmoja hivyo kukamilika kwake kutatoa fursa kwa wanafunzi wengi zaidi kujiunga na fani ya ufugaji nyuki. Mkuu amedokeza kuwa kupitia mradi huo mbali na wanafunzi kuongezeka chuoni hapo pia utasaidia kufa...

WILAYA YA LUSHOTO YAPOKEA MRADI WQ USAMBAZAJI NA UUZAJI WA MITUNGI YA GESI KWA BEI YA RUZUKU.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Lushoto - Tanga.  WANANCHI wa Wilaya ya Lushoto wamepata fursa mpya ya kunufaika na nishati safi ya kupikia baada ya wilaya hiyo kupokea rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).  Mradi huo umepokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Mheshimiwa Zephania Sumaye, kwa niaba ya wananchi wa wilaya hiyo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuhakikisha nishati safi ya kupikia inawafikia Watanzania wengi zaidi. Hafla ya mapokezi ya mradi huo imefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Lushoto na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, maafisa kutoka REA pamoja na wawakilishi wa kampuni ya Manjis Logistics Limited, ambayo imepewa jukumu la kutekeleza mradi huo kwa kushirikiana na REA. Mradi huo ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na REA nchini kwa lengo la kuharakisha upatikanaji wa nishati safi na salama kwa wananchi, kupunguza utegemezi wa kuni ...

ZAIDI YA WAKULIMA 200 WA ZAO LA PAMBA WAFUNGUA AKAUNTI IGUNGA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Igunga.  ZAIDI ya wakulima 200 wa zao la pamba kutoka vijiji vya Mwahalanga, Bukama, Mwabakima, Jogoya na Jilelabalimi vilivyopo katika Wilaya ya Igunga, Mkoa wa Tabora, wamefungua akaunti za benki na kusajili laini za simu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kupokea malipo ya mazao yao kwa njia ya kidijitali, hatua inayolenga kuongeza uwazi, usalama na uharaka wa malipo. Wakulima hao wamefungua akaunti kupitia Benki ya NMB pamoja na kusajili laini kupitia Mtandao wa simu wa Mixx by Yas, hatua ambayo itawawezesha kupokea fedha zao kwa urahisi kupitia mifumo ya benki na simu za mkononi. Ufunguzi wa akaunti hizo na usajili wa laini za simu unatekelezwa kufuatia maelekezo ya waraka wa Mrajis wa Vyama vya Ushirika unaozitaka AMCOS za wakulima wa pamba kuhakikisha malipo ya wakulima yanafanyika kupitia akaunti za benki na huduma za fedha kwa njia ya simu, badala ya kutumia mfumo wa malipo ya fedha taslimu (cash).  Lengo la hatua hiyo ni kuongeza uwazi, usalam...