Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba 3, 2025

TCAA YAWEZESHA MAFANIKIO YA REKODI YA DUNIA NDANI YA HIFADHI YA TARANGIRE.

Picha
Na Lubango Mleka, Tarangire. MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imeratibu na kusimamia kwa mafanikio safari ya kihistoria ya puto la hewa moto (hot air balloon) iliyoifanya Tanzania kuorodheshwa rasmi kama nchi ya 123 katika jaribio la rekodi ya dunia la kurusha balloon na rubani akiwa pekee yake, lililoendeshwa na Dkt. Rubani Allie Dunnington. Safari hiyo maalum imefanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Tarangire ikiwa ni mara ya kwanza kwa safari ya aina hii kufanyika na mtu mmoja ndani ya eneo la hifadhi. Uamuzi huu wa kipekee ulifikiwa na TCAA baada ya kufanya tathmini ya kina ya kiusalama, utaratibu wa kiufundi na uhalali wa operesheni ndani ya eneo hilo nyeti. Kwa mujibu wa TCAA, safari hiyo imefuata kikamilifu kanuni, taratibu na viwango vya usalama vya kitaifa na kimataifa. TCAA imeshirikiana kwa karibu na wadau wa uhifadhi pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kuhakikisha zoezi linafanyika kwa usalama, ufanisi na kulinda uadilifu wa mazingira ya hifadhi. Dkt. Ruba...

RACHEL NJAU AMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAPATIA WANAWAKE LESENI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MAKAMU Mwenyekiti wa chama cha wachimbaji madini wanawake Tanzania (TAWOMA) Rachel Joseph Njau amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kuwapatia wanawak leseni za uchimbaji na ununuzi wa madini bila malipo. Hivi karibuni Waziri wa Madini Anthony Mavunde aliwapatia leseni ya uchimbaji madini na leseni ya ununuzi wa madini wanawake na vijana 423 waliopo katika vikundi 21 wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara. Rachel ambaye pia ni Katibu wa chama cha wachimbaji madini Mkoa wa Manyara (MAREMA) Tawi la Mirerani ametoa shukrani hizo kwenye uchaguzi wa TAWOMA Tawi la Mirerani ambapo Magreth Nelson alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa TAWOMA kwa wanawake wafanyabiashara wa magonga ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite. Ameeleza kwamba kitendo cha Rais Samia Suluhu Hassan kuwasaidia wanawake kwenye mpango huo kinaongeza idadi ya wanawake wanaonufaika na sekta ya madini. "Tunampongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kumtuma Waziri Ant...

MAGE NELSON MWENYEKITI MPYA TAWOMA MIRERANI

Picha
  Na Mwandishi wetu, Mirerani  MFANYABIASHARA maarufu wa kuongeza thamani madini ya Tanzanite wa mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Magreth Nelson amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa chama cha wanawake wanaojihusisha na shughuli za madini Tanzania (TAWOMA) Tawi la Mirerani. Mage atatumikia kwa muda wa miaka mitano nafasi hiyo ya Mwenyekiti wa wanawake wafanyabiashara wa magonga ndani ya ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite mji mdogo wa Mirerani. Katika uchaguzi huo uliofanyika chini ya Makamu Mwenyekiti wa TAWOMA, Rachel Joseph Njau na Katibu Mkuu wa TAWOMA, Salma Ernest Kundi na kusimamiwa na Mwenyekiti wa MAREMA Tawi la Komolo Swalehe Abdalah na mjumbe wa MAREMA Tawi la Mirerani Jafar Matimbwa na kushuhudiwa na Afisa maendeleo ya jamii mamlaka ya mji mdogo wa Mirerani Floriana Mcharo. Mwenyekiti wa MAREMA Tawi la Komolo, Swalehe Abdalah akitangaza matokeo hayo amesema Magreth Nelson ambaye hakuwa na mpinzani alishinda nafasi hiyo kwa kupata kura ...