Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 1, 2026

DIAMOND AAHIDI VYOMBO VYAKE KUFUATA MATAKWA YA SHERIA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam. MKURUGENZI wa Wasafi Media, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz, ameipongeza Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kwa utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, huku akiahidi kuwa tayari kufuata matakwa yote ya kisheria yanayohusu sekta ya habari na watumishi wake.  Akizungumza baada ya kufika katika ofisi za Bodi hiyo tarehe 31 Januari, 2026 jijinj Dar es Salaam kwa ajili ya kupata ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya kisheria, Diamond amesema Wasafi Media haina nia ya kukwepa utekelezaji wa Sheria, bali iko tayari kushirikiana kikamilifu na wasimamizi wa taaluma hiyo. Amesema licha ya Sheria ya Huduma za Habari kuathiri vyombo vya habari kwa namna moja au nyingine, haiwezi kupingwa kwani ilitoa muda wa kutosha kwa wadau kujipanga na kutimiza vigezo vilivyowekwa ikiwemo Waandishi wake kuwa na kiwango cha Elimu cha Diploma na kuendelea. Diamond amekiri kuwa ujio wa Bodi ya Ithibati umeleta nidhamu kubwa katika t...

SERIKALI YAENDELEA KUWEKEZA MAFUNZO YA UJUZI BOBEZI KWA WATAALAM SEKTA YA AFYA

Picha
  Na WAF, Kibiti. SERIKALI kupitia Wizara ya Afya imeendelea kufanya uwekezaji kwenye sekta ya afya kwa hususan ni kwa wataalam Bingwa na  Bobezi ili wananchi wapate huduma bora za afya. Hayo yamebainishwa leo Januari 31, 2026 na Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kibiti, Dkt. Dismas Masulubu wakati wa zoezi la kuwajengea uwezo wataalam wa afya wanaotoa huduma za dharura (EMD) na huduma kwa wagonjwa mahututi (ICU). "Mafunzo haya yatawasaidia wataalam kumudu kuwahudumia wagonjwa mahututi kwa ufanisi pamoja na kutoa huduma za dharura kwa weledi zaidi. Pia yatawawezesha kutumia ipasavyo vifaa na mashine za kisasa zilizonunuliwa na Serikali kwa ajili ya kuimarisha huduma hizo" amesema Dkt. Masulubu. Dkt. Masulubu ametimia wasaa huo kuwashukuru wataalam kutoka Wizara ya Afya waliofika hospitalini hapo kutoa mafunzo, akisisitiza kuwa hatua hiyo itahakikisha wananchi wa Kibiti wanapata huduma bora za dharura na uangalizi wa wagonjwa mahututi karibu na makazi yao. Kwa upande wake, Mganga Mfawi...

DC NYAMWESE: MADIWANI MSITANGULIZE MASLAHI BINAFSI KWENYE HALMASHAURI

Picha
Asisitiza uwajibikaji, uwazi na ubunifu katika kuongeza mapato. Na Augusta Njoji, Handeni. MKUU wa Wilaya ya Handeni, Mhe. Salum Nyamwese, amewataka madiwani wa Halmashauri ya Mji Handeni, Halmashauri ya Wilaya ya Handeni na Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi kuacha kutanguliza maslahi binafsi au ya kisiasa wanapotekeleza majukumu yao, na badala yake kuweka mbele maslahi ya wananchi na maendeleo ya halmashauri. Nyamwese ametoa wito huo mjini Handeni wakati akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo madiwani, yaliyolenga kuwaimarisha katika masuala ya utawala bora, ufuatiliaji wa mapato na uelewa wa mipaka ya majukumu yao katika uendeshaji wa halmashauri. Amesisitiza kuwa serikali haitavumilia uzembe, hujuma wala vitendo vyovyote vinavyozorotesha maendeleo ya halmashauri, akiwataka madiwani kuwa macho na kutoa taarifa kwa wakati pindi wanapobaini mianya ya upotevu wa mapato. “Tunaomba mkawe wabunifu na mzishauri halmashauri namna bora ya kuboresha na kusimamia vyanzo vya mapato. Nyie ndio mnaoi...