Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 10, 2026

WAKUU WA IDARA NA VITENGO IGUNGA WAGAWIWA VISHIKWAMBI ILI KUACHANA NA MATUMIZI YA KARATASI.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Igunga. WAKUU wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora,  wamegawiwa Vishikwambi kwa lengo la kuvitumia katika vikao mbalimbali na kuachana na matumizi ya karatasi. Akizungumza baada ya kuwagawia vishikwambi hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Selwa Hamid amesema wanaendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika matumizi ya kidijitali. Amesema hatua hiyo, inaendelea kuondoa  mnyororo wa matumizi ya karatasi ambazo hutengenezwa kwa miti, hivyo kuendelea kutunza miti kwa mazigira rafiki kwa mwanadamu. Aidha, amewataka wakuu hao wa Idara na Vitengo kuvitumia vishikwambi hivyo kuongeza ufanisi wa kazi huku akiwasihi kutojaza picha na taarifa zisizohusiana na Menejimenti.

TEITI YAIMARISHA ELIMU KWA UMMA KUHUSU MANUFAA YA RASILIMALI ZA MADINI NA GESI

Picha
Na.Mwandishi Wetu. Taasisi ya Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) imesema imeendelea kuhimiza uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa rasilimali za nchi, ili kuhakikisha wananchi wananufaika na shughuli za uchimbaji na utafutaji. Akizungumza  jana katika mahojiano maalum,Katibu Mtendaji wa TEITI, Bi. Mariam Mgaya, amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi 57 zinazotekeleza viwango vya kimataifa vya uwazi na uwajibikaji vinavyosimamiwa na EITI. Amesema Tanzania ilijiunga na EITI mwaka 2009, hatua iliyolenga kuimarisha usimamizi bora wa rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia kwa maslahi ya maendeleo endelevu. “Asasi hii inahamasisha wananchi kuelewa hatua zote za mnyororo wa thamani wa rasilimali hizi, ikiwemo ukusanyaji na ufuatiliaji wa mapato,” amesema Bi.Mgaya Bi. Mgaya amebainisha kuwa utekelezaji wa majukumu ya TEITI unasimamiwa na Sheria ya TEITA ya mwaka 2015 ambayo imeainisha jukumu la kuboresha uwazi na uwajibikaji, hasa katika uvunaj...