Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi 25, 2026

TAKUKURU, TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA YASAINI MIKATABA YA KUDHIBITI RUSHWA.

Picha
  Na Hamida Ramadhan,  Dodoma.  TAASISI  ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa kushirikiana na Tume ya Maendeleo ya Ushirika zimesaini makubaliano ya ushirikiano yatakayolenga kuzuia na kupambana na vitendo vya rushwa katika vyama vya ushirika nchini.  Hatua hiyo inalenga kuimarisha uwajibikaji, uwazi na kurejesha imani ya wanachama wa ushirika. Akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa makubaliano hayo, Msajili na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika, Dkt. Benson Ndiege, alisema sekta ya ushirika imekuwa ikikabiliwa na changamoto za usimamizi wa rasilimali, ambazo kwa kiasi kikubwa zimechangiwa na vitendo vya rushwa. Alieleza kuwa wanachama wengi wamekuwa wakiweka fedha, mazao na rasilimali zao katika vyama vya ushirika kwa matarajio ya kunufaika, lakini vitendo vya rushwa vimekuwa vikikwamisha malengo hayo na kupunguza imani yao. “Ushirikiano huu unalenga kukomesha vitendo vya rushwa na kurejesha matumaini ya wanachama tumejipanga kuhakik...

REA YAENDELEZA MAPINDUZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KOROGWE.

Picha
  Wananchi Wanufaika na usambazaji na uuzaji wa Mitungi ya Gesi kwa bei ya ruzuku.  Na Mwandishi Wetu, Korogwe - Tanga.  WANANCHI wa wilaya ya Korogwe mkoani Tanga  wameanza kuona mwanga mpya wa maisha kufuatia kuendelea kwa mpango wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).  Mpango huo unaolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia, umeleta matumaini mapya kwa kaya nyingi zilizokuwa zikitegemea kuni na mkaa. Katika muendelezo wa zoezi hilo, REA imeendelea kusambaza mitungi ya gesi kwa gharama nafuu, hatua inayolenga kuhakikisha hata wananchi wa kipato cha chini wanapata fursa ya kutumia nishati salama na rafiki kwa mazingira.  Akizungumza wakati wa zoezi hilo, Msimamizi wa mradi kutoka REA, Ndugu Abdulrazack Mkomi ameeleza kuwa jitihada hizo ni sehemu ya mkakati mpana wa serikali wa kupunguza utegemezi wa nishati za jadi ambazo zimekuwa zikichangia uharibifu wa mazi...

RAIS SAMIA ALETA NEEMA KWA MABINTI WALIOKOSA ELIMU SIKONGE

Picha
Na Allan Kitwe, Sikonge MABINTI zaidi ya 34 waliokosa fursa ya kupata elimu ya sekondari Wilayani Sikonge Mkoani Tabora wameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwapa fursa ya kupata elimu hiyo kwa miaka miwili pasipo kulipa gharama yoyote. Mabinti hao ambao wengi wao walikatishwa masomo kwa sababu mbalimbali ikiwemo hali duni ya maisha ya wazazi wao, kupata ujauzito, kukatishwa masomo ili waozeshwe katika umri mdogo na mtizamo hasi wa wazazi wao kuhusu elimu. Wakizungumza na waandishi wa habari waliotembelea Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Wilayani humo jana walimshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fursa kwa watoto wa kike waliokosa elimu kurudi shuleni. Watoto hao licha ya kupata fursa ya kusoma elimu ya sekondari bure kwa miaka 2 (QT) pia wanasoma masomo ya ufundi stadi ambapo kila mmoja anasoma fani anayopenda, hii inampa fursa ya kupata elimu ya sekondari na ujuzi wa ufundi pia. Miracle Mvungu (25) kutoka Kata ya Igigwa Wilayani humo ameeleza kuwa baada ya kumal...

BREAKING NEWS: - WAZIRI LUKUVI AFARIKI DUNIANI

Picha