Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba 27, 2025

PET SCAN IANZE KUFANYA KAZI OCEAN ROAD- DKT SHEKALAGHE

Picha
Na. Lubango Mleka, Dar es Salaam. KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Seif Shekalaghe, ameuagiza uongozi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road na mkandarasi anayesimika kifaa tiba cha PET Scan kuhakikisha wanakamilisha usimikaji wa kifaa hicho ndani ya muda waliokubaliana. Dkt. Shekalaghe ametoa agizo hilo Novemba 25, 2025, wakati wa ziara yake ya ukaguzi wa utoaji wa huduma katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, jijini Dar es Salaam. “Tumekubaliana kwamba hadi siku ya Ijumaa, mkandarasi anatakiwa kumpatia Mkurugenzi wa Ocean Road uhakiki wa benki (Bank Guarantee) ili Mkurugenzi aweze kumlipa asilimia 75 ya malipo yake. Hii itamwezesha mkandarasi kufanya maandalizi ya kuhakikisha PET Scan inaanza kufanya kazi. Wataalam wamenishauri kuwa baada ya hapo tutahitaji siku 30 kwa ajili ya maandalizi ya mashine hiyo kuzalisha mionzi tiba kwa ajili ya kugundua kansa,” amesema Dkt. Shekalaghe. Aidha, amewahakikishia wananchi wanaofika hospitalini hapo kupata huduma, kuwa Serikali imenunua galimu ...

WAANDISHI WA HABARI NI WADAU MUHIMU KATIKA KUIMARISHA AMANI, USALAMA NA UTULIVU WA TAIFA

Picha
Na Lubango Mleka, Dodoma. NAIBU Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Dennis Lazaro Londo, amewahakikishia waandishi wa habari nchini kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wao wa kujieleza pamoja na kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kwa usalama na weledi. Mhe. Londo amezungumza hayo leo Novemba 27, 2025 jijini Dodoma katika mafunzo ya waandishi wa habari yaliyowaleta pamoja Wanahabari 100 kutoka maeneo mbalimbali nchini, Mhe. Londo amesema Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi itaendelea kushirikiana na wadau wa habari katika maeneo yote yanayohusu usalama kwa waandishi wa habari. Aidha, amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msukumo mkubwa katika kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi, sambamba na kulinda uhuru wa vyombo vya habari.  " Falsafa ya Mhe. Rais kupitia “4R” zinaipa tasnia ya habari nafasi muhimu katika kulinda amani, kuimarisha umoja wa kitaifa na kuendeleza mijadala yenye tija kwa jamii." Am...

MNADA WA KOROSHO MOROGORO

Picha
 

KANISA LA FPCT LAIPONGEZA SERIKALI KUSOGEZA HUDUMA ZA MOYO KWA WANANCHI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Nkinga - Igunga. KANISA la FPCT Jimbo la Nzega limeipongeza Serikali ya awamu 6 chini ya Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa ujio wa Madaktari Bingwa Bobezi wa Moyo walioweka Kambi ya matibabu ya Moyo Hospitali ya Rufaa ya Nkinga Igunga. Pongezi hizo zimetolewa leo na Askofu Ezekiel Silasi wa Jimbo la Nzega alipotembelea Hospitali ya Rufaa ya Nkinga ili kuona jinsi huduma za kambi zinavyotolewa kwa wananchi. "Ujio wao umeleta tija kubwa katika jamii yetu lakini kwa Kanisa la FPCT, tunasikia kuthaminiwa sana, binafsi kwaniaba ya Askofu Mkuu niwashukuru sana Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa kuja hapa Nkinga kutuletea huduma hii lakini pia kuwapa uzoefu Madaktari wetu." Ameongeza, "Ushirikiano huu uendelee kwa sababu Afya za watanzania zikiimarika hayo ndio maendeleo ya nchi yetu" amesema Askofu Silasi. Bw.Omary Kalonga mkazi wa kata ya Magengati wilayani Nzega ameipongeza Hospitali ya Rufaa ya Nkinga kuwaleta Madaktari hao kwani ingewagharimu fedha nying...