Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 17, 2026

VETA YAONESHA BIDHAA ZINAZOTENGENEZWA NA WANAFUNZI WAKATI WA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imetumia maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kuonesha bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na wanafunzi wake, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha jamii kutambua mchango wa mafunzo ya ufundi stadi katika maendeleo ya kiuchumi. Akizungumza katika maonesho hayo, Meneja wa Rasilimali Watu wa VETA, Eliaika Manyanga, akimwakilisha Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, alisema bidhaa zinazooneshwa zimetengenezwa na wanafunzi kwa kushirikiana na walimu wao kupitia mafunzo ya vitendo yanayotolewa katika vyuo vya VETA. Alisema bidhaa hizo zinajumuisha vifaa mbalimbali vya matumizi ya nyumbani na ofisini vinavyotumiwa na makundi tofauti ya jamii, huku vikionesha kiwango cha ujuzi na ubunifu unaopatikana kwa wahitimu wa taasisi hiyo. Manyanga alisema VETA inaendelea kutoa mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu yanayolenga kuwawezesha vijana kujiajiri na kuajirika, huku akibainisha kuwa udahili wa wanafunzi kwa muhula ...

ASMA MWINYI FOUNDATION YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU

Picha
  Na Jasmine Shamwepu, Dodoma.  MWANZILISHI na Mkurugenzi wa Taasisi ya Asma Mwinyi Foundation, ambaye pia ni Mbunge wa Welezo, Unguja, Asma Ally Hassan Mwinyi, ameungana na watoto wenye usonji (Autism), ugonjwa wa Down Syndrome na mtindio wa ubongo (Cerebral Palsy), pamoja na wazazi wao, kuadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika kwa kuwapa fursa ya kusikika na kujadili changamoto zinazowakabili. Katika maadhimisho hayo ya Juni 16, Asma Mwinyi Foundation kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe iliandaa ziara maalumu ya watoto hao na wazazi wao katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma, ambapo walipata nafasi ya kuzungumza na viongozi na kueleza changamoto wanazokabiliana nazo katika maisha ya kila siku. Akizungumza wakati wa shughuli hiyo, Asma alisema lengo la kuwakutanisha watoto hao na wazazi wao ni kuendelea kutoa elimu kwa jamii, kuondoa unyanyapaa na kuhamasisha upatikanaji wa huduma bora za afya na matibabu kwa watoto wenye mahitaji...

WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA YAHIMIZA VIJANA KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WAZIRI ya Viwanda na Biashara imewahimiza wananchi, hususan vijana na wajasiriamali, kutumia kikamilifu fursa zinazotolewa na taasisi zake ili kukuza biashara, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya uchumi wa taifa. Wito huo umetolewa leo Juni 17, 2026 na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Saidi Msabimana, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma. Msabimana amesema wizara hiyo, ambayo ni miongoni mwa taasisi muhimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, imeshiriki maonesho hayo pamoja na taasisi nane zilizo chini yake kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi pamoja na kutoa elimu kuhusu biashara, viwanda na uwekezaji. Amesema jukwaa hilo limetumika kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuwapa taarifa za huduma zinazotolewa na kuwaelekeza namna ya kutumia fursa zilizopo kwa maendeleo yao binafsi na taifa kwa ujumla. “Tunatumia jukwaa hili ku...

NBS YAONA TAKWIMU NI NGUZO MUHIMU YA UTEKELEZAJI WA DIRA 2050

Picha
Na Hamida Ramadhan, Dodoma.  OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema takwimu rasmi zitakuwa nyenzo muhimu katika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 inayolenga kuifikisha Tanzania katika uchumi wa dola trilioni moja na kuongeza kipato cha wananchi. Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa NBS, Daniel Masolwa, alisema hayo wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma, ambapo taasisi hiyo inashiriki kutoa elimu kwa wananchi kuhusu huduma na majukumu yake. Masolwa amesema kaulimbiu ya mwaka huu inayosema “Kuchochea Uwajibikaji Jumuishi kwa Huduma Endelevu” imeipa NBS fursa ya kueleza umuhimu wa takwimu rasmi katika kupanga maendeleo, kufanya maamuzi sahihi na kufuatilia utekelezaji wa mipango mbalimbali ya taifa. Amesema kwa mujibu wa Sheria ya Takwimu, Sura ya 351, NBS imepewa mamlaka ya kukusanya, kuchakata na kusambaza takwimu rasmi zinazotumika katika sekta mbalimbali za maendeleo. “Takwimu rasmi ni msingi wa upangaji ...

WANANCHI WATAKIWA KUHESHIMU HAKI ZA WATOTO

Picha
Na. Wellu Mtaki, Dodoma.  Wazazi na walezi wamehimizwa kuwalea watoto katika maadili mema ili kuwaepusha na tabia za kuiga zisizofaa ambazo zinaweza kuwaletea madhara katika maisha yao.  Sambamba na hilo, wananchi wametakiwa kutambua na kuheshimu haki za watoto ili kuhakikisha wanakua katika mazingira salama na yenye upendo. Kauli hiyo imetolewa na Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Faithmary Lukindo, alipokuwa akimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Eliakim Chacha Maswi, katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Kituo cha Malezi ya Watoto Kikombo jijini Dodoma. Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa kijiji, viongozi wa dini, wastaafu pamoja na waimbaji wa Kwaya ya Gethsemane. Akizungumza katika hafla hiyo, Lukindo alisema mtoto anapopewa haki ya kusikilizwa na kutoa maoni yake, hujengewa hali ya kujiamini na kujiona mwenye thamani ndani ya familia na jamii inayomzungu...