Na Hamida Ramadhan, Dodoma. MWENYEKITI wa Bunge Bonanza, Festo Sanga, amesema washiriki wa Bunge Bonanza wanatarajiwa kujitolea kuchangia damu salama kwa hiari katika tukio litakalofanyika Jumamosi, Januari 31, 2026, kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari John Merlin Miyuji jijini Dodoma. Akiongea na waandishi wa habari leo Januari 29 ,2026 Bungeni jijini Dodoma Sanga amesema zoezi hilo lina lengo la kuokoa maisha ya wagonjwa, kupunguza dharura za kiafya na kuimarisha mshikamano wa kijamii kati ya washiriki na jamii kwa ujumla. Ameeleza kuwa kuchangia damu ni kitendo cha huruma kinachoongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa afya na mshikamano wa kitaifa. Amesema Bunge Bonanza linahusisha mashindano ya michezo ya burudani ikiwemo mpira wa miguu, kuruka kamba, pete, mashindano ya kula, kufukuza kuku pamoja na michezo mingine yenye lengo la burudani na mshikamano. Ameongeza kuwa tukio hilo litawakutanisha mashabiki wa timu za soka za Simba na Yanga, washiriki kutoka vyuo...