Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 9, 2026

POLISI YAWASAKA WANAWAKE WALIOMSHAMBULIA MWENZAO KWA MWIKO

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  JESHI la Polisi nchini Tanzania limesema limeanza kufanya uchunguzi kuhusiana na picha mjengeo inayosambazwa kupitia mitandao ya kijamii wakionekana wanawake wawili wakimpiga mwanamke mmoja kwa kutumia mwiko na kumshambulia kwa maneno kwa madai ya kudhalilishwa na mhanga wa tukio hilo kupitia mtandao Facebook. Taarifa ya Polisi iliyotolewa leo Jumatatu Februari 09, 2026 na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, (DCP) David Misime imeeleza kuwa katika Picha hiyo mjongeo, wanawake hao wamesikika wakihoji sababu za mmoja wao kudhalilishwa kwenye Mitandao ya kijamii kuwa amekuwa akiiba mabwana (Waume) za watu.  Jeshi la Polisi kupitia taarifa yake hiyo limetoa wito kwa yeyote anayewafahamu wanawake hao kuwasilisha taarifa zao kwa njia anayoona inafaa na rahisi kwake ili kuweza kuwafikia na kuwakamata ili kuwachukulia hatua za kisheria.

DHAMIRA YA RAIS SAMIA NI KUHAKIKISHA HUDUMA BORA ZA AFYA KWA WANANCHI

Picha
Na WAF-Dar es Salaam Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imedhamiria kuhakikisha tabasamu la Watanzania linaendelea kuonekana kwa kuboresha huduma za afya nchini. Dkt. Samizi amesema hayo jijini Dar es Salaam wakati akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya anayeshughulikia Dawa na Vifaa Tiba, Bw. Emmanuel Tayari, aliporipoti katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Afya. Amesema kuongezwa kwa Bw. Tayari katika timu ya uongozi wa Wizara kutaongeza nguvu na uimara katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara, hususan katika kuhakikisha huduma bora za afya, upatikanaji wa dawa na vifaa tiba unaimarika, na hivyo kuweka tabasamu kwa wananchi. “Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imelenga kuona Watanzania wanapata huduma bora za afya, jambo litakalowezesha tabasamu la wananchi kuonekana na kudumu, sambamba na kutekeleza azma ya Serikali na Dira ya Taifa ya Maendel...

JAMII YAHIMIZWA KUACHA UNYANYAPAA KWA WATU WANAOISHI NA KIFAFA

Picha
  Na WAF-Dar es Salaam  NAIBU Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi (Mb), ametoa wito kwa Watanzania kuacha unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na ugonjwa wa kifafa na kuchukua hatua madhubuti za kuboresha upatikanaji wa huduma bora za matibabu kuanzia ngazi ya msingi. Dkt. Samizi ametoa wito huo leo Februari 9, 2026 jijini Dar es Salaam wakati akifungua rasmi Maadhimisho ya Siku ya Kifafa Duniani pamoja na Mkutano wa Kifafa Nchini ulioandaliwa na Chama cha Kifafa Tanzania (TEA), uliofanyika katika Ukumbi wa Ummy Mwalimu, Hospitali ya Taifa Muhimbili. Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa, Naibu Waziri amesema ugonjwa wa kifafa bado umezungukwa na imani potofu katika jamii nyingi, hali inayosababisha wagonjwa wengi kuchelewa kupata matibabu sahihi na kukumbana na changamoto za kijamii, kisaikolojia na kiuchumi. “Katika baadhi ya jamii, kifafa huaminika kuwa ni ugonjwa unaoambukiza au unaosababishwa na uchawi, jambo linalopelekea wagonjwa kunyanya...

NAIBU KATIBU MKUU MPYA WA WIZARA YA FEDHA, BW. NSUBILIN JOSHUA ALAKIWA OFISI NDOGO ZA WIZARA YA FEDHA DAR ES SALAAM

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, atakayekuwa anashughulikia masuala ya Utawala (Huduma za Hazina), Bw. Nsubili Joshua, akipokelewa na Viongozi na baadhi ya Watumishi wa Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam baada ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kushika wadhifa huo. Ikulu Jijini Dar es Salaam. Baada ya kuwasili, Bw. Joshua alilakiwa na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, ambaye pia ni Naibu Waziri anaye simamia Sera za Uchumi, Bw. Elijah Mwandumbya, na baadae kukaribishwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), ambaye alifanya kikao kifupi na Naibu Katibu Mkuu mpya, pamoja na viongozi na wafanyakazi wa Ofisi Ndogo ya Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam. Bw. Nsubuli Joshua, anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu-Huduma za Hazina, Bi. Jenifa Omolo, ambaye aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Su...

RAIS SAMIA APELEKA TABASAMU SIKONGE

Picha
  Na Allan Kitwe, Sikonge.  RAIS wa Awamu ya Sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan amepeleka tabasamu kwa wakazi wa Wilaya ya Sikonge Mkoani Tabora baada ya maji safi na salama kutoka Ziwa Viktoria kufika Wilayani humo. Shangwe na furaha za wananchi zimelipuka kwenye hafla ya kufungulia maji hayo iliyofanyika juzi katika Kata ya Misheni Mjini Sikonge kwenye eneo lilipojengwa tanki kubwa la kupokelea maji hayo ili yaanze kusambazwa kwa wananchi. Akizungumza na mamia ya wananchi, wadau wa maendeleo na viongozi mbalimbali wa chama na serikali kwenye hafla hiyo, Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Aweso ameeleza kufurahishwa na kazi nzuri ya utekelezaji mradi huo. Amesema kuwa mradi huo ambao unatekelezwa na Mkandarasi kutoka China kwa gharama ya shilingi bilioni 143 umelenga kufikisha huduma ya maji safi na salama katika Wilaya tatu za Urambo, Kaliua na Sikonge yenyewe. ‘Ndugu zangu wana Sikonge, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameleta tabasamu kwenu, alipoingi...

JIMMY LAI AFUNGWA MIAKA 20 JELA KWA KUUNGA DEMOKRASIA.

Picha
  Hong Kong - China. MAHAKAMA ya Hong Kong imemhukumu bilionea anayefahamika kwa kuunga mkono demokrasia, Jimmy Lai, kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya ukiukaji wa usalama wa taifa mwezi Desemba. Hukumu hiyo ndiyo kali zaidi kuwahi kutolewa chini ya sheria tata ya usalama wa taifa, ambayo China inadai ni muhimu kwa uthabiti wa jiji hilo. Lai, mwenye pasipoti ya Uingereza, alikuwa miongoni mwa wakosoaji wakubwa wa Beijing, akitumia mara kwa mara gazeti lake la kidemokrasia Apple Daily kama chombo cha kupinga utawala huo. Wakuu sita wa zamani wa gazeti hilo pia wamehukumiwa kifungo cha jela siku ya Jumatatu, kati ya miaka sita na miezi tisa hadi miaka 10. Kwa wanaharakati wa demokrasia, Lai anaonekana kama shujaa, lakini kwa Beijing anachukuliwa kuwa msaliti. Amekuwa akikanusha mashtaka yote dhidi yake, akisema alitetea kile alichoamini kuwa ni maadili ya Hong Kong, ikiwemo utawala wa sheria na uhuru wa kujieleza. Hukumu hiyo ina maana kuwa huenda aka...