Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 9, 2026

ENABEL YAWEZESHA MABINTI 200 KASULU KUPATA ELIMU

Picha
  Na Allan Kitwe, Kasulu.  SHIRIKA la Maendeleo la Ubelegiji (ENABEL) limeunga mkono juhudi za serikali kwa kuwezesha watoto wa kike zaidi ya 200 Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma kupata mafunzo ya ujuzi katika Chuo Cha Maendeleo ya Wananchi Kasulu (FDC). Hayo yamebainishwa jana na Mkuu wa Chuo hicho Fridegarda Mukyanuzi alipokuwa akiongea na waandishi wa habari Ofisini kwake ambapo ameeleza kufurahishwa na ujio wa mradi huo ili kuwezesha wasichana wasio na uwezo. Amebainisha kuwa kupitia mradi huo Shirika limegharamia mahitaji yote ya Chuo kwa watoto hao na kuwawezesha kusoma fani mbalimbali za ufundi ikiwemo ushonaji nguo, ususi na urembo, umeme wa majumbani na ufundi bomba. Fani nyingine ni ufundi magari, uchomeleaji na uungaji vyuma, umeme wa magari na wa majumbani na kila wanapohitimu Shirika huwawezesha vifaa vya kuanzia shughuli zao. Amefafanua kuwa mradi huo wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 600 umekuwa mkombozi kwa Chuo na kwa watoto hao kwani umesaidia kuboresha...