Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari 16, 2026

MBUNGE AGNES MARWA ATOA SADAKA MAALUM KUUNGA MKONO MAANDALIZI YA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Musoma.  MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Mara, Agnes Marwa, leo ametoa sadaka maalum kwa viongozi wa dini ya Kiislamu katika Misikiti tofauti ya Musoma Mjini ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono maandalizi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Sadaka hiyo imelenga kuwasaidia viongozi wa dini pamoja na waumini katika kujiandaa na mwezi huo muhimu wa ibada, unaoheshimiwa na Waislamu duniani kote. Baadhi ya vitu vilivyotolewa ni pamoja na buswati, tende, kanzu, balaghashee pamoja na fedha taslimu, ambavyo vimekabidhiwa kwa viongozi kutoka misikiti mbalimbali ya Musoma Mjini. Akizungumza wakati wa tukio hilo, Agnes Marwa alisema kuwa sadaka hiyo ni ishara ya mshikamano, upendo na heshima kwa viongozi wa dini, pamoja na kuthamini mchango wao katika kujenga maadili mema na amani ndani ya jamii. “Nimeona ni muhimu kushiriki na ndugu zetu wa Kiislamu katika maandalizi ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Huu ni mwezi wa ibada, subira, na kusaidiana, hivyo ni wajibu wetu kama viongozi kuende...

WATU WAWILI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA MAUAJI YA MWENYEKITI WA CCM TAWI LA ITUMBI MBEYA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Mbeya.  KUPITIA mitandao ya kijamii kunasambazwa picha mjongeo akionekana mtu mmoja mwanaume ambaye anajinasibu kuhusika katika tukio la mauaji ya aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Tawi la Itumbi aitwaye Elia Richard Sambala, miaka 53, mkazi wa Itumbi Wilaya ya Chunya Mkoa wa Mbeya. Ukweli ni kwamba, Februari 11,2026 saa 7 mchana katika Kijiji cha Itumbi, Elia Richard Sambala, alikutwa shambani kwake akiwa amejeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye makali kichwani na watu wasiojulikana na alifariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa Hospitali ya Wilaya ya Chunya kwa matibabu. Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya, kupitia Askari wa kuchunguza matukio ya mauaji, walianza msako mkali na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa wawili kuhusiana na tukio hilo na ufuatiliaji zaidi kwa wengine waliohusika unaendelea. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa, chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa masilahi wa eneo la uchimbaji madini ya dhahabu ambapo mmoja wa wanafamilia hao alikodi...

MATUMIZI YA KONDOMU YASHUKA KWA ASILIMIA TANO: KENGELE YA TAHADHARI KWA TAIFA

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dodoma.  WAKATI  dunia ikiendelea kupaza sauti kuhusu umuhimu wa kinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na magonjwa ya zinaa, takwimu zinaonesha kuwa matumizi ya kondomu nchini yameshuka kwa takribani asilimia tano.  Hii si namba ya kupuuzwa ni ishara inayopaswa kuamsha mjadala mpana na hatua za haraka katika kulinda afya ya jamii. Kupungua huku kunakuja licha ya kampeni za muda mrefu za uhamasishaji na upatikanaji wa kondomu katika vituo vya afya na maeneo mbalimbali ya umma.  Je, tatizo ni nini? Je, ni uchovu wa kampeni, kuongezeka kwa dhana potofu, au kupungua kwa hofu ya maambukizi kutokana na maendeleo ya tiba? Baadhi ya wananchi wa Dodoma wanasema bado kuna pengo la elimu sahihi kuhusu matumizi ya kondomu. Ingawa asilimia hiyo inaweza kuonekana ndogo kwa mtazamo wa haraka, kwa tathmini ya afya ya umma ni takwimu yenye uzito mkubwa.  Kupungua huku kunamaanisha kuwa watu zaidi wako katika hatari ya kuambukizwa au wanawake ku...