NCHIMBI AAGIZA VIONGOZI WANAOWAKWAMISHA WAANDISHI WAENDESHA OFISI KUCHUKULIWA HATUA
Na Happyness Hans, WAF - ARUSHA MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe.Dkt. Emmanuel Nchimbi amewataka viongozi na wakuu wa Idara wanaowazuia waandishi waendesha Ofisi kushiriki mikutano ya chama hicho kuchukuliwa hatua za kinidhamu. Amesema hayo leo Mei 21, 2026 Mkoani Arusha kwa niaba ya Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan wakati akifungua rasmi Mkutano Mkuu wa 13 wa Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA), unaoambatana na uchaguzi wa viongozi wapya wa chama hicho. “Tunatamani kila kiongozi awapende, awajali, awape safari, motisha na kuwapongeza pale wanapofanya vizuri,” amesema Dkt. Nchimbi. Mhe. Dkt. Nchimbi amesema Ofisi yoyote bila uwepo wa waandishi waendesha Ofisi ni sawa na gari lisilo na usukani, kwani wao ndiyo sura na lango la Ofisi. Amesema hakuna mtu anayeweza kuonana moja kwa moja na kiongozi bila kupitia kwa mwendesha Ofisi. Aidha amesema waandishi waendesha Ofisi wamekuwa msaada mkubwa katika Taasisi mbalim...