Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari 20, 2026

WIZARA YA VIJANA NA MICHEZO YAIMARISHA USHIRIKIANO WA TIBA YA MICHEZO NA TANZANIA

Picha
Na Lubango Mleka. WIZARA ya Vijana na Michezo katika kusaidia na kuendeleza mfumo wa tiba ya michezo,  chini ya ufadhili wa Dkt. Ashraf Sobhy, Waziri wa Vijana na Michezo, na usimamizi wa Kamati Kuu ya Tiba ya Wizara, inayoongozwa na Profesa Dkt. Hazem Khamis, Kituo cha Olimpiki cha Maadi kimepokea ujumbe kutoka Taasisi ya Moyo ya Tanzania (JKCI) katika ziara maalum. Ujumbe huo umejumuisha Mkurugenzi  wa Hospitali ya JKCI, Dar Group Dkt. Tulizo Shemu , Dkt. Tatizo Waane, Mkurugenzi wa Idara ya Magonjwa ya Moyo JKCI na Dkt. Eva Michel, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa Watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete JKCI. Ziara hiyo iliandaliwa kwa ushirikiano na uratibu na Jumuiya ya Misri na Afrika ya Utafiti na Magonjwa ya Moyo, inayoongozwa na Profesa Dkt. Ahmed Ashraf Issa; Jumuiya ya Kiarabu - Ushirikiano wa Afrika, inayoongozwa na Balozi Mohamed Lagouzi; na Chama cha "Kutoka Moyoni hadi Moyoni", kinachoongozwa na Profesa Dkt. Ghada Qazamel. Ujumbe huo pia ulijumuisha ...

FCC, ZFCC ZAJADILI UIMARISHAJI WA USHINDANI WA BIASHARA NA KUMLINDA MLAJI

Picha
Na Mwandishi wetu. KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amefanya ziara ya kikazi katika Tume ya Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar (ZFCC) ikiwa ni hatua ya kuimarisha mashirikiano kati ya taasisi hizo mbili katika masuala ya ushindani, ulinzi wa mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia. Bi. Ngasongwa alipokelewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZFCC, Bi. Aliya Juma ambapo viongozi hao walifanya mazungumzo kuhusu kuendeleza ustawi wa taasisi hizo na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Akizungumza katika ziara hiyo iliyofanyika tarehe 14 Januari, 2026 katika ofisi za ZFCC - Zanzibar, Bi. Ngasongwa alisema ushirikiano kati ya taasisi hizo unaendelea kuimarika kupitia utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (MoU) yaliyokwisha sainiwa. "FCC na ZFCC tayari zimeanza kutekeleza kwa vitendo maeneo ya ushirikiano ikiwemo kujengeana uwezo, kubadilishana uzoefu na kufanya ukaguzi wa pamoja ili kudhibiti bidhaa bandia na kulinda haki za watumiaji wa bidh...

WANASWA KWA KUHUJUMU MRADI WA MAJI WA MIJI 28

Picha
  Na Allan Kitwe, Tabora. WATU wanne wamekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Tabora kwa tuhuma za kuhujumu Mradi wa Maji wa Miji 28 unaoendelea kutekelezwa na serikali katika Wilaya za Sikonge, Urambo na Kaliua ili kumaliza kero ya wananchi. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoani hapa ACP Constatine Mbogambi amethibitisha kukamatwa watuhumiwa hao wakiwa na vifaa mbalimbali vilivyoibiwa kwenye mradi huo Wilayani Urambo. Ametaja baadhi ya vifaa vilivyokamatwa kuwa ni mashine kubwa 3 za kuchomelea mabomba, grenda mashine 2 za kukatia mabomba, nyaya 9 za kuunganishia grenda hizo na lita 40 za mafuta ya mitambo ya hydroliki. Kamanda amefafanua kuwa vifaa hivyo viliibiwa usiku wa tarehe 11 Januari 2026 Wilayani Urambo katika eneo la mradi huo mkubwa wa maji kutoka ziwa Victoria ambao unatekelezwa na serikali kwa gharama ya zaidi ya sh bil 143. ‘Baada ya kuibiwa mashine na vifaa hivyo, vilisafirishwa na kwenda kufichwa katika Kitongoji cha Ubalani-Majengo, Mjini Urambo tayari kwa ajili ya kutafuta ...

MAMA AJIFUNGUA NA KUTELEKEZA KICHANGA GESTI

Picha
  Na Allan Kitwe, Nzega. MWANAMKE mmoja ambaye jina halijajulikana amejifungua mtoto na kumtelekeza kwenye nyumba ya kulala wageni (gesti) Wilayani Nzega Mkoani Tabora na kutokomea kusikojulikana. Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Mkuu wa Wilaya hiyo Naitapwak Tukai ameeleza kusikitishwa na tukio hilo na kuahidi kutoa donge nono la shilingi 500,000 kwa mtu yeyote atakayesaidia kupatikana mwanamke huyo. Alieleza kuwa kitendo hicho hakikubaliki katika jamii na ni ukatili wa hali ya juu, kama huyo mama aliweza kukaa na mimba kwa miezi yote tisa na kujifungua salama iweje amtupe mtoto gesti?, alihoji. ‘Naomba mtu yeyote mwenye taarifa za mwanamke aliyekuwa mjamzito na sasa haonekani kuwa na mtoto atoe taarifa Kituo cha Polisi au aje kwa Mkuu wa Wilaya moja kwa moja anipe taarifa, hatutamtaja kokote’, alisema. DC alibainisha kuwa mtoto anakadiriwa kuwa na umri wa siku 3 tu tangu azaliwe, hivyo kumtelekeza namna hii ni kumnyima haki yake ya msingi ya kunyonya maziwa ya mama, kupata m...

KAPINGA AWASHUKURU WANANCHI KATA YA MKAKO NA KIHANGIMAHUKI, AHAHIDI USHIRIKIANO WA KARIBU KUTATUA CHANGAMOTO ZAO.

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Mbinga. MBUNGE wa Jimbo la Mbinga Vijijini na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Salvio Kapinga, ametembelea Kata za Mkako na Kihangimahuka katika mwendelezo wa ziara yake ya kuwashukuru wananchi kwa ushindi mkubwa waliompatia yeye na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Lihale, Mhe. Kapinga aliahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu na Serikali ya Wilaya pamoja na taasisi husika ili kutatua changamoto zinazowakabili wananchi, hususan katika sekta za miundombinu, maji na umeme. “Serikali ipo pamoja nanyi, na mimi kama Mbunge wenu nitaendelea kushirikiana na viongozi wa wilaya na taasisi zote kuhakikisha changamoto zenu zinapatiwa ufumbuzi wa kudumu". Katika kuonesha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya elimu, Mhe. Kapinga alitoa msaada wa bati 50 za geji 28 zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 1.7 pamoja na kiasi cha shilingi laki tano kwa ajili ya ununuzi wa kenchi...