Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba 7, 2025

WANANCHI WA KATEMBE, MWALONI MULEBA WAONDOKANA NA ADHA YA BARABARA

Picha
*Ni kiunganishi cha wafanyabiashara wa Rwanda, Burundi na Uganda* Na Mwandishi Wetu, Muleba.  UJENZI wa barabara ya lami ya Katembe -Mwaloni inayounganisha Barabara kuu ya kutoka nchi za Uganda, Rwanda na Burundi katika wilaya ya Muleba  Mkoani Kagera  uliogharimu zaidi ya shilingi Milioni 400 umeleta ahueni kwa wakazi wa eneo hilo pamoja na wafanyabiashara wa samaki kutoka katika visiwa vilivyopo ndani ya ziwa Victoria kwenda ndani na nje ya Nchi. Kiongozi wa mbio za Mwenge  wa uhuru Kitaifa Ndugu Ismail  Ussi ameridhisha na viwango vya mradi huo na kuwapongeza TARURA kwa utekelezaji wa mradi wenye viwango ambao unaendeleaa kuwasaidia wananchi . Alisema kuwa Ili wanachi wapate huduma bora na nguvu ya kuzalisha wanahitaji Barabara nzuri zenye viwango na kupitia umma wa wananchi ameshukuru usimamizi wa mradi huo na namna Halmashauri ya Muleba ulivyotoa mapato ya ndani kujenga Barabara imara inayoweza  kuchochea uchumi na kuvutia wawekezaji na wafanyabiashara...

WAZIRI WA HABARI ZANZIBAR ANUNUA TIKETI 100 MCHEZO WA NIGER NA TANZANIA

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar.  WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mh: Tabia Maulid Mwita, amenunua Tiketi 100, kwa ajili ya Mashabiki, Kushuhudia Mchezo Kati ya Timu ya Taifa ya Tanzania dhidi ya Niger. #tabiamwita #r.hmwinyi #wizara_ya_habari_zanzibarz #Tanzania #Niger

TRA YAKARIBISHWA MAKANISANI KUTOA ELIMU YA KODI

Picha
Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro.  MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Kilimanjaro imealikwa kutoa elimu ya kodi kwa Wanachama wa ELCT SACCOS katika kikao cha mwaka cha taasisi hiyo.  Mafunzo hayo yamefanyika jana tarehe 06.09.2025 katika Kanisa  la KKKT ushirika wa Majengo , katika manispaa ya Moshi, Mwika na Hai  mkoani Kilimanjaro ambapo mada  zilizowasilishwa ni pamoja na Usajili wa biashara mtandaoni, Dawati maalumu la uwezeshaji biashara na uwasilishaji wa ritani za kodi na ulipaji wa kodi kwa hiari. Akiwasilisha mada, Afisa Msimamizi wa Kodi Mwandamizi, Bw. Odupoi Papaa amewasisitiza wanachama kuwasilisha ritani za kodi na kufanya ya kodi kwa wakati pamoja na kutoa na kudai risiti za kielektroniki.