Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni 12, 2026

ZFCT YARIDHISHWA NA MAFUNZO YA FCC KUHUSU USIMAMIZI WA MASHAURI YA USHINDANI

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Dar Es Salaam.  BARAZA la Ushindani Halali Zanzibar (ZFCT) limefanya ziara ya mafunzo katika Tume ya Ushindani ya Haki (FCC) kwa lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu katika masuala ya ushindani wa biashara, udhibiti wa bidhaa bandia pamoja na usimamizi wa mashauri yanayohusiana na ushindani. Ziara hiyo iliyofanyika katika ofisi za FCC Juni 10, 2026 Jijini Dar es Salaam, imeelezwa kuwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi hizo mbili ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuhakikisha mazingira ya biashara yanakuwa ya haki kwa wadau wote. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Khadija Ngasongwa alisema kuwa kubadilishana uzoefu na taasisi za ndani ya nchi ni muhimu katika kuimarisha mifumo ya usimamizi wa ushindani na kulinda maslahi ya watumiaji dhidi ya vitendo vinavyokiuka sheria za ushindani na biashara. Alisema ujumbe wa ZFCT unapata fursa ya kujifunza namna FCC inavyotekelez...

TCDC YATOA ELIMU YA MALIPO KWA NJIA YA BENKI NA SIMU WILAYA YA MEATU

Picha
Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC) imetoa mafunzo ya elimu kuhusu mfumo wa malipo ya zao la pamba kwa njia ya benki na simu katika Wilaya ya Meatu, mafunzo hayo yamehusisha Makatibu Mameneja, Wenyeviti na Makarani wa AMCOS 71 kutoka wilaya hiyo.