Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba 29, 2025

ROGHAT FALME ROBERT KUIWAKILISHA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA CHAKULA DUNIANI UNAOTARAJIWA FANYIKA NCHINI ITALY

Picha
C  CEO wa Shirika lisilo la Kiserikali la Akili Platform Tanzania, anatarajia kuondoka hapa nchini hivi karibuni kuelekea nchini Italy kwenye Mkutano wa chakula duniani unaotarajiwa kufantika Octoba, 10 -17, 2025.

DK.MWINYI AAHIDI UWEKEZAJI MKUBWA BWAWANI NA KUIMARISHA MJI MKONGWE

Picha
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar. MGOMNEA Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali ina mpango wa kufanya uwekezaji mkubwa katika eneo la Hoteli ya Bwawani katika awamu ijayo ya uongozi wake. Akizungumza katika mkutano wa kampeni Jimbo la Malindi, Mkoa wa Mjini Magharibi, leo tarehe 29 Septemba 2025, Dkt. Mwinyi alibainisha kuwa eneo hilo ni muhimu kwa uchumi na utalii wa Zanzibar, na Serikali inalenga kulibadilisha kuwa mfano bora wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Aidha, ameeleza kuwa Serikali ya awamu ijayo pia itatekeleza mpango maalum wa kuimarisha nyumba zote za Mji Mkongwe zikiwemo nyumba za wakfu, binafsi na za Serikali ili ziendelee kudumu kwa muda mrefu, kwa kutumia fedha za ndani. Kuhusu changamoto ya magari kuingia Mji Mkongwe, amesema Serikali imekamilisha mpango wa mabasi ya umeme ili kupunguza tatizo hilo na kulinda uimara wa majengo ya kihistoria. ...

DK.MWINYI AAHIDI KUJENGA MASOKO MAPYA 5 ZANZIBAR

Picha
  Na Mwandishi Wetu, Zanzibar. MGOMBEA wa Nafasi ya Rais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameahidi kujenga masoko makubwa mapya matano ili kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao katika mazingira bora zaidi. Akizungumza na wafanyabiashara wa Soko la Mwanakwerekwe leo tarehe 29, Septemba 2025 katika muendelezo wa kampeni za uchaguzi, Dkt. Mwinyi alisema masoko hayo mapya yatakayojengwa katika maeneo ya Kinyasini, Mwera, Kibandamaiti, Kisauni na Kwahajitumbo yataleta suluhisho la kudumu kwa changamoto za wafanyabiashara. Ameeleza kuwa kukamilika kwa masoko hayo kutapunguza msongamano unaotokana na uhaba wa nafasi, pamoja na kupunguza kodi kubwa zinazowakabili wafanyabiashara hivi sasa. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amewaomba wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kumchagua tena yeye pamoja na wagombea wa CCM katika ngazi za ubunge, uwakilishi na udiwani, ili kutimiza dhamira...

UCSAF YAKAMILISHA MINARA 734, UJENZI WAFIKIA ASILIMIA 96.83.

Picha
  UJENZI wa minara 758 ya mawasiliano unaosimamiwa na Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) umefikia hatua kubwa ya mafanikio, ambapo minara 734 tayari imekamilika na inatoa huduma za mawasiliano kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya vijijini nchini. Hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 96.83, hali inayodhihirisha dhamira ya Serikali kupitia UCSAF kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za mawasiliano, hususan wale wa maeneo ya vijijini na yenye changamoto za kijiografia. Minara iliyosalia ni 24 pekee, na inatarajiwa kukamilika hivi karibuni ili kuhakikisha huduma za mawasiliano zinafika katika maeneo yote yaliyopangwa. Mradi huu ni matokeo ya ushirikiano mzuri kati ya Serikali na kampuni za simu nchini kwa lengo la kufikisha huduma za mawasiliano vijijini, zikiwemo huduma za intaneti na simu ambazo zimekuwa changamoto katika maeneo yaliyokuwa hayana mtandao wa uhakika. Wananchi wa vijiji ambavyo minara imekamilika wameshaanza kunufaika na mawasiliano bora...

MATHIAS CANAL AONGOZA UPATIKANAJI MIL 85 UJENZI WA KANISA KIOMBOI-IRAMBA.

Picha
Na Mwandishi Wetu, Iramba. MWANZIRISHI na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya WAZOHURU MEDIA Ndg Mathias Canal amewaongoza Viongozi wa dini, Wadau wa maendeleo na Waumini kwenye harambee ya ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania-KKKT Usharika wa St George Kiomboi Wilaya ya Iramba Mkoani Singida. Katika harambee hiyo iliyofanyika jana tarehe 28 Septemba 2025 katika eneo la Ujenzi wa Kanisa Mtaa wa Lulumba, Mgeni huyo rasmi amesimamia upatikanaji wa fedha taslimu Tsh 79,407,000 ambapo ahadi ni Shilingi Milioni 4,010,000 na jumla ya fedha zote zilizopatikana ni Shilingi Milioni 85,017,000. Mgeni rasmi Ndg Mathias Canal pamoja na marafiki zake waliomuunga mkono amechangia jumla ya Tsh milioni 3,835,000 na mifuko 10 ya Saruji. Akizungumza katika harambee hiyo Mathias amesema kuwa Kanisa ni nguzo muhimu ya maisha ya kiroho, kijamii na hata kiuchumi. Kupitia kanisa waumini wanajifunza misingi ya upendo, mshikamano, uadilifu na ujenzi imara wa taifa.  "Ujenzi wa kanisa si kwa aj...

TANGAZO.

Picha
OFISI YA MKUU WA WILAYA YA IGUNGA IKISHIRIKIANA NA OFISI YA MKURUGENZI MTENDAJI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA IGUNGA ANAWATANGAZIA WANANCHI WOTE KUWA, Hospitali ya Wilaya Igunga inategemea kupokea timu ya madaktari Bingwa wa Mh.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuanzia tarehe  29/09/2025  hadi tarehe 03/10/2025. Madaktari Bingwa watakaokuwepo ni 01. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya wanawake( kinamam) 02. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya ndani (mfano kisukari,pressure nk) 03. Daktari Bingwa wa Upasuaji  04. Daktari Bingwa wa magonjwa ya kinywa na meno 05. Daktari Bingwa wa watoto  06. Daktari Bingwa wa Usingizi na ganzi 07. Muuguzi mbobezi. Wananchi wote wenye uhitaji wa huduma hizo wafike Hospitali ya Wilaya Igunga. Huduma zitatolewa kwa gharama nafuu kabisa. NYOTE MNAKARIBISHWA.

TANZANIA YAENDELEZA USHINDI KATIKA MASHINDANO YA ICC MEN’S T20 WORLD CUP AFRICA QUALIFIER, 2025.

Picha
  Na Mwandishi Wetu,Zimbabwe. BALOZI wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. CP. Suzan S. Kaganda, ameongoza maafisa wa Ubalozi kushuhudia Timu ya Taifa ya Cricket ya Tanzania katika mchezo wa mashindano ya ICC Men’s T20 World Cup Africa Qualifier 2025, uliofanyika tarehe 28 Septemba 2025, kati ya Tanzania na Uganda. Katika mchezo huo uliofanyika kwenye viwanja vya Takashinga vilivyopo mjini Harare, Zimbabwe, Timu ya Taifa ya Cricket ya Tanzania imeibuka mshindi baada ya kuifunga timu ya Uganda kwa runs 9, hatua inayofanya timu ya Tanzania kuendelea na ushindi baada ya kuifunga timu ya Taifa ya Botswana siku ya Ijumaa, tarehe 26 Septemba 2025. Ushindi huu ni mafanikio muhimu katika ICC Men’s T20 World Cup Africa Qualifier 2025. Kufuatia ushindi huo dhidi ya Uganda, timu ya Tanzania kwa sasa imefuzu kuingia hatua ya nusu fainali. Mchezo wa nusu fainali utachezwa mnamo tarehe 02 Oktoba 2025, kati ya Tanzania na Namibia kwenye uwanja uliopo mjini Harare, Zimbabwe. Ubalozi wa Tanzania unaend...